Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

49

Malkia Muovu Anapata Malipizi

Malkia Muovu Anapata Malipizi

Kupitia dirisha la nyumba yake ya kifalme, mufalme Ahabu angeweza kuona shamba la mizabibu la mwanaume mwenye aliitwa Naboti. Alipenda lile shamba na alipenda kuliuza. Lakini Naboti alikataa kuuzishalile shamba juu Sheria ya Yehova ilikataza mutu kuuzisha shamba lenye aliriti. Ahabu aliheshimia Naboti juu alitii Sheria ya Yehova? Hapana. Ahabu alikasirika sana. Alikasirika sana mupaka hakukuwa anapenda kutoka mu chumba chake. Alikuwa anakataa hata kula.

Yezebeli, malkia muovu, akaambia bwana yake Ahabu hivi: ‘Wewe njo mufalme wa Israeli. Unaweza kupata kila kitu chenye unapenda. Nitakupatialile shamba, litakuwa lako.’ Kisha Yezebeli akaandikia wazee wa muji barua. Akawaambia hivi: “Mushitaki Naboti. Museme ametukana Mungu. Kisha mumupige majiwe akufe.” Wazee wakafanya vile. Halafu Yezebeli akaambia Ahabu: ‘Naboti alishakufa. Sasa lile shamba la mizabibu linakuwa lako.’

Haiko Naboti tu njo mwenye Yezebeli aliua. Aliua watu mingi wenye hawakukuwa na kosa na wenye walimupenda Yehova. Tena, Yezebeli aliabudu sanamu na alifanya mambo ingine ya mubaya. Lakini Yehova alikuwa anaona mambo yote ya mubaya yenye Yezebeli alikuwa anafanya. Yehova angemufanya Yezebeli nini?

Wakati Ahabu alikufa, Yehoramu, mutoto wake, akakuwa mufalme. Kisha Yehova akatuma mwanaume mwenye aliitwa Yehu apatie Yezebeli na familia yake malipizi.

Yehu alipanda mu gari, na akaenda Yezreeli, kwenye Yezebeli alikuwa anaishi. Yehoramu akaenda na gari lake juu amupokee Yehu. Wakati alikutana naye, akamuuliza: ‘Kuko amani kati yetu?’ Yehu akamujibu: ‘Hakuwezi kuwa amani wakati Yezebeli mama yako angali anatenda mambo ya mubaya.’ Yehoramu akatafuta kugeuza gari lake juu akimbie. Lakini Yehu akamutupia mushale, na Yehoramu akakufa.

Kisha Yehu akaenda ku nyumba ya kifalme kwenye Yezebeli alikuwa. Wakati Yezebeli alisikia kama Yehu iko anakuja, akajipamba, akatengeneza nywele, kisha akamungojea ku sehemu ya juu ya nyumba, na alikuwa anamuangalia kupitia dirisha. Wakati Yehu alifika, Yezebeli akamuambia maneno ya kumuzarau. Yehu akalalamika na kuambia watumishi wa Yezebeli wenye walikuwa pembeni yake: ‘Mumutupe chini!’ Wakamutupa chini kupitia dirisha. Akaanguka na kufa.

Kisha, Yehu akaua watoto wanaume 70 wa Ahabu na akafanya ibada ya Baali iishe mu inchi yote. Hadisi hii inatufundisha nini? Inatufundisha kama Yehova anaonaka kila kitu, na kwa wakati wenye kufaa, anapatiaka malipizi wale wenye wanafanyaka mambo ya mubaya.

“Uriti wenye unapatikana kwanza kwa pupa mwishowe hautakuwa baraka.”​—Mezali 20:21