Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

50

Yehova Anasaidia Yehoshafati

Yehova Anasaidia Yehoshafati

Yehoshafati, mufalme wa Yuda, alibomoa mazabahu na sanamu za Baali mu inchi yote. Alipenda watu wajue sheria za Yehova. Kwa hiyo, alituma wakubwa na Walawi mu inchi yote ya Yuda juu wafundishe watu sheria za Yehova.

Mataifa ya karibu-karibu iliogopa kupigana na Yuda kwa sababu ilijua kama Yehova alikuwa pamoja na watu wake. Hata ile mataifa ililetea Mufalme Yehoshafati zawadi. Lakini siku moja, Wamoabu, Waamoni, na wakaaji wa eneo la Seiri walikuja kupigana na Yuda. Yehoshafati alijua kama alikuwa na lazima ya musaada wa Yehova. Alikusanya pamoja wanaume, wanamuke, na watoto wote Yerusalemu. Kisha Yehoshafati alisali hivi mbele yao: ‘Yehova, bila wewe, hatuwezi kushinda hii vita. Tafazali utuambie kama tufanye nini.’

Yehova alijibu ile sala. Aliwaambia: ‘Musiogope. Nitawasaidia. Kila mutu asimame fasi yake. Musitikisike. Mujionee namna nitawaokoa.’ Yehova aliwaokoa namna gani?

Asubui ya siku yenye ilifuata, Yehoshafati akachagua waimbaji na kuwaambia wakuwe mbele ya jeshi. Walitembea kutoka Yerusalemu mupaka ku uwanja wa vita, wenye ulikuwa fasi kwenye kunaitwa Tekoa.

Wakati waimbaji walikuwa wanamusifu Yehova kwa sauti kubwa na kwa furaha, Yehova alipigania watu wake. Alifanya kukuwe muvurugo kati ya Waamoni na Wamoabu. Walianza kupigana wao kwa wao, na hakuna mutu mwenye aliokoka. Lakini Yehova alilinda watu wa Yuda, maaskari, na makuhani. Watu wote wa inchi za karibu-karibu walisikia mambo yote yenye Yehova alifanya. Na walielewa kama Yehova angali analinda watu wake. Namna gani Yehova anaokoaka watu wake? Anatumia njia mingi. Hana lazima ya musaada wa wanadamu ili kufanya vile.

“Hamutakuwa na lazima ya kupigana pigano hili. Musimame mahali penu, musimame bila kutikisika, na muone wokovu wa Yehova kwa ajili yenu.”​—2 Mambo ya Nyakati 20:17