Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 52

Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto

Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto

Mfalme Ben-hadadi wa Siria alikuwa akivamia Israeli mara kwa mara. Lakini kila mara nabii Elisha alikuwa akimwonya mfalme wa Israeli, hivyo alikuwa akiponyoka. Kwa hiyo, Ben-hadadi akaamua kumteka Elisha. Alijulishwa kwamba Elisha alikuwa katika jiji la Dothani, basi akalituma jeshi la Siria kumkamata.

Wasiria wakafika Dothani usiku. Asubuhi iliyofuata, mtumishi wa Elisha akaenda nje naye akaona kwamba jiji lilikuwa limezingirwa na jeshi kubwa. Akaogopa sana naye akapaaza sauti akisema: ‘Elisha, tutafanya nini?’ Elisha akamwambia hivi: ‘Wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.’ Mara moja Yehova akamfanya mtumishi wa Elisha aone kwamba milima yote kuzunguka jiji hilo ilikuwa imejaa farasi na magari ya vita ya moto.

Askari-jeshi Wasiria walipojaribu kumkamata Elisha, akasali hivi: ‘Yehova, tafadhali wapige kwa upofu.’ Ghafla, ingawa bado wangeweza kuona, askari hao hawakujua walipokuwa. Elisha akawaambia askari hao: ‘Mmekuja kwenye jiji lisilofaa. Nifuateni, nitawapeleka kwa mwanamume mnayemtafuta.’ Wakamfuata Elisha hadi Samaria, ambako mfalme wa Israeli aliishi.

Wasiria walipogundua mahali walipokuwa, ilikuwa kuchelewa mno. Mfalme wa Israeli akamuuliza Elisha: ‘Je, niwaue?’ Je, Elisha alitumia nafasi hiyo kulipiza kisasi watu waliokuwa wamejaribu kumuumiza? Hapana. Elisha alisema hivi: ‘Usiwaue. Wape chakula na uwaache waondoke.’ Kwa hiyo, mfalme akawaandalia karamu kubwa na kuwaruhusu waende nyumbani.

“Huu ndio uhakika tulio nao kwake, kwamba tukiomba chochote kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.”​—1 Yohana 5:14