Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

52

Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto

Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto

Ben-hadadi, Mufalme wa Siria, alikuwa anashambulia Israeli mara mingi. Lakini kila mara nabii Elisha alikuwa anajulisha mufalme wa Israeli, kwa hiyo alikuwa anakimbia. Basi, Ben-hadadi aliamua kukamata Elisha kinguvu. Walimujulisha kama Elisha iko mu muji wa Dotani, basi alituma maaskari wa Siria kule ili wamukamate.

Wasiria walifika Dotani usiku. Asubui, mutumishi wa Elisha alienda inje na akaona kama maaskari mingi walikuwa wamezunguka muji. Akaogopa sana. Kisha, akasema hivi kwa sauti kubwa: ‘Elisha, tutafanya nini?’ Elisha akamuambia: ‘Wale wenye kuwa pamoja na sisi ni wengi kuliko wale wenye kuwa pamoja nao.’ Mara moja Yehova akafanya mutumishi wa Elisha aone namna milima yote ya pembeni-pembeni ilikuwa imejaa farasi na magari ya vita ya moto.

Wakati maaskari Wasiria walitafuta kukamata Elisha, akasali hivi: ‘Tafazali Yehova, uwafanye wakuwe vipofu.’ Mara moja, wale maaskari, hata kama walikuwa wanaona, hawakujua kama walikuwa wapi. Kisha, Elisha akawaambia: ‘Mulishapotea. Munifuate, nitawapeleka kwa ule mwenye muko munatafuta.’ Wakafuata Elisha mupaka Samaria, kwenye mufalme wa Israeli alikuwa anaishi.

Wakati Wasiria walivumbua kwenye walikuwa, hakukuwa kitu chenye wangeweza kufanya. Mufalme wa Israeli akauliza Elisha: ‘Niwaue?’ Unawaza, Elisha alitumia ile nafasi ili kulipiza kisasi watu wenye walijaribu kumufanya mubaya? Hapana. Elisha aliambia Mufalme wa Israeli: ‘Usiwaue. Uwapatie chakula na uwaache waende.’ Kwa hiyo, mufalme akawafanyia karamu kubwa na akawaacha warudie kwao.

“Huu ndio uhakika wenye tuko nao kwake, kwamba hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.”​—1 Yohana 5:14