Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

54

Yehova Alivumilia Yona

Yehova Alivumilia Yona

Watu wenye waliishi Ashuru mu muji wa Ninawi, walikuwa wabaya sana. Yehova aliambia nabii wake Yona aende kule ili awaambie kama wanapaswa kubadilika na kuacha mwenendo wao. Lakini Yona alikimbia na kuenda fasi ingine. Aliingia mu mashua (bateau) ya kuenda Tarshishi.

Wakati mashua ilikuwa inaenda, kulitokea upepo mukubwa mu bahari. Wenye kutumika mu mashua waliogopa sana. Walisali kwa miungu yao na kuiuliza: ‘Juu ya nini hii upepo inatokea?’ Kisha, Yona akawaambia: ‘Ni kosa langu. Nilikimbia kazi yenye Yehova alinipatia. Munitupe mu bahari, na upepo utaisha.’ Wale watu hawakupenda kutupa Yona mu bahari, lakini aliwakaza wamutupe. Wakati walimutupa mu bahari, ule upepo ukaisha.

Yona aliwaza kama atakufa. Wakati alianza kuzama, alisali kwa Yehova. Kisha Yehova alituma samaki mukubwa sana. Ile samaki ikamumeza Yona, lakini haikumuua. Yona alisali hivi wakati alikuwa ndani ya tumbo la samaki: ‘Ninakuahidi kama nitakutii sikuzote.’ Yehova alilinda Yona ndani ya ile samaki kwa siku tatu. Kisha, alifanya ile samaki imutapike ku inchi kavu.

Kwa sababu Yehova aliokoa Yona, ni kusema haikukuwa tena lazima aende Ninawi? Hapana. Yehova aliambia tena Yona aende Ninawi. Yona alitii. Alienda na kuambia wakaaji wa Ninawi hivi: ‘Kisha siku 40, Ninawi itaharibiwa.’ Lakini jambo fulani la kushangaza lilitokea: Watu wa Ninawi walisikiliza na wakabadilisha mwenendo wao. Mufalme wa Ninawi aliambia watu wake hivi: ‘Muombe Mungu, na mutubu. Pengine hatatuharibu.’ Wakati Yehova aliona kama watu wametubu, hakuharibu muji wa Ninawi.

Yona alikasirika juu Yehova hakuharibu Ninawi. Waza kidogo: Yehova alivumilia Yona na alimuhurumia, lakini Yona hakutaka kuhurumia watu wa Ninawi. Alienda inje ya muji wa Ninawi, na akakaa chini ya kivuli cha mumea wa mutango. Kisha ule mutango ukakauka, na Yona akakasirika sana. Yehova akamuambia: ‘Unahangaikia huu mumea kupita vile unahangaikia watu wa Ninawi. Niliwahurumia, njo maana sikuwaharibu.’ Yehova alipenda kufundisha Yona nini? Watu wa Ninawi walikuwa wa maana kupita mumea wa mutango.

“Yehova . . . ni muvumilivu kuwaelekea ninyi kwa sababu hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.”​—2 Petro 3:9