Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

55

Malaika wa Yehova Alilinda Hezekia

Malaika wa Yehova Alilinda Hezekia

Ashuru ilikuwa imeshinda ufalme wa makabila kumi ya Israeli. Sasa Senakeribu, mufalme wa Ashuru, alitaka kushinda ufalme wa Yuda wa makabila mbili. Akaanza kukamata miji ya Yuda, moja kisha ingine. Na Yerusalemu njo muji wenye alipenda sana kukamata. Lakini, hakujua kama Yehova alikuwa analinda Yerusalemu.

Hezekia, mufalme wa Yuda, alipatia Senakeribu feza mingi juu asikamate Yerusalemu. Senakeribu alikamata zile feza, lakini alituma maaskari wake wenye nguvu wakamate Yerusalemu. Watu wa Yerusalemu waliogopa sana juu Waashuru walikuwa wanakaribia sana. Lakini Hezekia aliwaambia: ‘Musiogope. Waashuru wako na nguvu, lakini Yehova atatufanya tukuwe na nguvu kuwapita.’

Senakeribu alituma mujumbe wake, Rabshake, aende kuchekelea watu wa Yerusalemu. Rabshake alisimama inje ya muji na kusema hivi kwa sauti kubwa: ‘Yehova hawezi kuwasaidia. Hezekia asiwadanganye. Hakuna mungu mwenye anaweza kuwalinda.’

Hezekia aliomba Yehova amuambie jambo la kufanya. Yehova alimujibu hivi: ‘Usiogope mambo yenye Rabshake anasema. Senakeribu hatakamata Yerusalemu.’ Kisha, Senakeribu alitumia Hezekia barua fulani. Zile Barua zilisema hivi: ‘Muitike tu tukamate Yerusalemu. Yehova hawezi kuwaokoa.’ Hezekia alisali hivi: ‘Tafazali, Yehova, utuokoe ili kila mutu ajue kama wewe tu njo Mungu wa kweli.’ Yehova alimujibu hivi: ‘Mufalme wa Ashuru hataingia Yerusalemu. Nitalinda muji wangu.’

Senakeribu alikuwa hakika kama atakamata Yerusalemu. Lakini usiku moja, Yehova alituma malaika fasi kwenye maaskari Waashuru walikuwa wametia kambi yao, inje ya muji. Ule malaika aliua maaskari 185000! Mufalme Senakeribu alipoteza maaskari wake wenye nguvu sana. Hakukuwa na jambo lingine la kufanya, isipokuwa tu kurudia kwake. Yehova alilinda Hezekia na muji wa Yerusalemu, sawa vile alikuwa ametoa ahadi. Kama ungekuwa Yerusalemu ile wakati, ungemutumainia Yehova?

“Malaika wa Yehova anapiga kambi pande zote kuzunguka wale wenye kumuogopa Yeye, na anawaokoa.” ​—Zaburi 34:7