Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

57

Yehova Anatuma Yeremia Aende Kuhubiri

Yehova Anatuma Yeremia Aende Kuhubiri

Yehova alichagua Yeremia akuwe nabii. Alimuomba aende kuhubiria watu wa Yuda na awaambie kama walipaswa kuacha kufanya mambo ya mubaya. Lakini Yeremia akasema: ‘Yehova, niko kijana mudogo tu. Sitaweza kuzungumuza na watu.’ Yehova akamuambia: ‘Usiogope. Nitakuambia mambo ya kusema. Na nitakusaidia.’

Yehova aliambia Yeremia akusanye wanaume wazee, avunje chupa ya udongo mbele yao, na kusema: ‘Ni vile Yerusalemu itavunjwa.’ Wakati Yeremia alivunja ile mutungi sawa vile Yehova alikuwa amemuambia, wale wazee walikasirika sana. Kuhani mwenye aliitwa Pashuri akamupiga Yeremia na kutia mikono na miguu ya Yeremia mu mikatale. Usiku wote, Yeremia hakuweza kutoka pale. Asubui ya siku yenye ilifuata, wakati Pashuri alimufungua, Yeremia alisema: ‘Sitaweza kuendelea. Nitaacha kuhubiri.’ Lakini, unawaza aliachaka kuhubiri? Hapana. Alifikiri sana juu ya uamuzi wake na akasema: ‘Maneno ya Yehova iko sawa vile moto wenye kuwaka ndani yangu. Sitaacha kuhubiri.’ Kwa hiyo, Yeremia aliendelea kuonya watu.

Miaka ikapita, na kukakuwa mufalme mwingine mu inchi ya Yuda. Makuhani na manabii wa uongo walichukia mambo yenye Yeremia alikuwa anahubiri. Waliambia wakubwa hivi: ‘Huyu mutu anastahili kufa.’ Lakini Yeremia akawaambia: ‘Kama munaniua, mujue kama munaua mutu mwenye hana kosa. Mambo yenye ninasema haiko yangu, ni ya Yehova.’ Wakati wakubwa walisikia vile, wakasema: ‘Huyu mutu hastahili kufa.’

Yeremia aliendelea kuhubiri, na wakubwa wakakasirika sana. Waliambia mufalme amuue. Lakini mufalme Sedekia aliwaambia wamufanye vile wanapenda. Basi wakamukamata na kumutupa mu kisima ya murefu mwenye mulikuwa matope, waliwaza kama atakufa mule. Yeremia akaanza kuzama ndani ya matope.

Kisha Ebed-meleki, mutumishi wa mufalme, akaambia mufalme: ‘Wakubwa wametupa Yeremia mu kisima! Kama tunamuacha mule, atakufa.’ Sedekia akaambia Ebed-meleki akamate wanaume 30, na watoshe Yeremia mu kile kisima. Sawa vile tumeona, Yeremia hakuruhusu jambo lolote limuzuie kuhubiri, hauone kama ni muzuri tufuate mufano wake?

“Mutachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu, lakini ule mwenye atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.”​—Matayo 10:22