Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

58

Yerusalemu Inaharibiwa

Yerusalemu Inaharibiwa

Mara mingi, watu wa Yuda walimuacha Yehova na kuanza kuabudu miungu ya uongo. Yehova alijaribu kuwasaidia kwa miaka mingi. Alituma manabii ili wawaonye. Lakini, kuliko kusikiliza wale manabii, waliwacheka. Yehova alifanya nini juu amalize kabisa ibada yao ya sanamu?

Nebukadneza, Mufalme wa Babiloni, alikuwa anashinda taifa moja kisha lingine. Wakati alishinda Yerusalemu mara ya kwanza, alikamata Mufalme Yehoyakini, wakubwa, wanaume wa vita, na mafundi, na akawapeleka Babiloni. Tena, alikamata mali yote yenye ilikuwa mu hekalu la Yehova. Kisha, Nebukadneza alifanya Sedekia kuwa mufalme wa Yuda.

Ku mwanzo, Sedekia alikuwa anatii Nebukadneza. Lakini, mataifa ya karibu-karibu na manabii wa uongo walimushauria Sedekia aasi utawala wa Babiloni. Yeremia alimuonya hivi: ‘Kama unaasi, kutakuwa vita, njaa, na magonjwa mu inchi ya Yuda.’

Kisha kutawala kwa miaka munane, Sedekia aliasi mufalme wa Babiloni. Aliomba maaskari wa Misri wamusaidie. Kisha Nebukadneza alituma maaskari wake wapigane na Yerusalemu. Wale maaskari walitia kambi yao karibu na Yerusalemu. Yeremia aliambia hivi Sedekia: ‘Yehova amesema, ukijitia mu mikono ya mufalme wa Babiloni, utaendelea kuishi, wewe na wakaaji wote wa muji. Lakini kama haufanye vile, Wababiloni watachoma Yerusalemu kwa moto na watakufunga.’ Sedekia akajibu: ‘Sitajitia mu mikono yake!’

Kisha mwaka moja na nusu, maaskari wa Babiloni walitoboa tundu kubwa mu ukuta wa Yerusalemu na wakaingia mu muji. Kisha walichoma kwa moto muji na hekalu, waliua na kufunga watu mingi.

Sedekia alikimbia Yerusalemu, lakini Wababiloni walimufuata. Wakamukamata karibu na muji wa Yeriko na kumuleta kwa Nebukadneza. Mufalme wa Babiloni aliua watoto wa Sedekia mbele ya macho ya Sedekia. Kisha akatoboa macho ya Sedekia na kumufunga mu gereza. Mule njo alikufiaka. Lakini Yehova alitoa ahadi hii kwa watu wa Yuda: ‘Kisha miaka 70, nitawarudisha kwenu Yerusalemu.’

Nini njo ilipata vijana wenye walipelekwa Babiloni? Waliendelea kuwa waaminifu kwa Yehova?

“Yehova Mungu, Mweza-Yote, hukumu zako ni za kweli na za haki.”​—Ufunuo 16:7