Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

59

Vijana Ine Wenye Walimutii Yehova

Vijana Ine Wenye Walimutii Yehova

Nebukadneza alipeleka wakubwa wa Yuda Babiloni, na aliomba Ashpenazi, mutumishi wake, awachunge. Nebukadneza aliambia Ashpenazi atafute kati yao vijana wenye afya ya muzuri na wenye akili sana. Wale vijana wangepewa mazoezi kwa miaka tatu. Ile mazoezi ingewafanya wakuwe watu wa maana sana mu inchi ya Babiloni. Wale vijana walipaswa kujifunza kusoma, kuandika, na kusema luga ya Kiakadi yenye watu walikuwa wanasema mu Babiloni. Walipaswa kula chakula ileile yenye mufalme na watumishi wake walikuwa wanakula. Kati yao, kulikuwa Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria. Ashpenazi aliwapatia majina ya Wababiloni. Aliita Danieli Belteshaza, Hanania akakuwa Shadraki, Mishaeli akakuwa Meshaki, na Azaria akakuwa Abednego. Unafikiri mambo yenye waliwafundisha ilifanya waache kumutumikia Yehova?

Wale vijana ine walipenda sana kumutii Yehova. Walijua kama hawakupaswa kula chakula ya mufalme sababu mufalme alikuwa anakula chakula fulani yenye Sheria ya Yehova ilikataza. Basi, waliambia Ashpenazi: ‘Tafazali, usitupatie chakula ya mufalme.’ Ashpenazi aliwaambia: ‘Kama hamukule chakula ya mufalme, na kisha anavumbua kama munaonekana kuwa wagonjwa, ataniua!’

Danieli akapata wazo fulani. Akaambia hivi mulinzi: ‘Tafazali, utupatie tu mboga za majani na maji, kwa siku kumi. Kisha, utatulinganisha na vijana wenye wako wanakula chakula ya mufalme.’ Ule mulinzi akaitika.

Kisha zile siku kumi, Danieli na marafiki wake watatu walionekana kuwa na afya ya muzuri kupita vijana wengine wote. Yehova alifurahi kuona namna walimutii. Hata alipatia Danieli hekima ya kuelewa maana ya maono na ndoto.

Wakati ile mazoezi iliisha, Ashpenazi alileta wale vijana mbele ya Nebukadneza. Mufalme alizungumuza nao na akaona kwamba Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria walikuwa na hekima na akili ya mingi kupita vijana wengine wote. Basi, akachagua wale vijana ine juu wafanye kazi mu nyumba yake ya Kifalme. Mara mingi, mufalme alikuwa anawaomba mashauri juu ya mambo ya lazima. Yehova alifanya wakuwe na hekima kupita watu wote wenye hekima wa mufalme na watu wote wenye kufanya uchawi.

Hata kama walikuwa mbali na kwao, Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria hawakusahau kama walikuwa watumishi wa Yehova. Na wewe, utakuwa muaminifu kwa Yehova, hata kama unajikuta mbali na wazazi wako?

“Usiruhusu hata kidogo mutu yeyote azarau ujana wako. Lakini, ukuwe mufano kwa waaminifu katika kusema, katika mwenendo, katika upendo, katika imani, na katika mwenendo safi.”​—1 Timoteo 4:12