Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

61

Walikataa Kuinamia Sanamu

Walikataa Kuinamia Sanamu

Wakati fulani kisha kulota ndoto ya ile sanamu, Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu kubwa ya zahabu. Aliisimamisha fasi kwenye hakukuwa milima, kwenye kuliitwa Dura. Aliita watu wa maana sana mu inchi wakusanyike mbele ya ile sanamu. Kati yao, kulikuwa Shadraki, Meshaki, na Abednego. Mufalme alisema hivi: ‘Wakati tu mutasikia sauti ya tarumbeta, vinubi, na zumari, muinamie ile sanamu! Mutu mwenye atakataa kuiinamia atatupwa ndani ya tanuru ya moto.’ Wale Waebrania watatu wangeinamia ile sanamu? Ao wangemuabudu Yehova tu?

Kisha mufalme akatoa amri watu wapige muziki. Watu wote wakainamia ile sanamu, lakini Shadraki, Meshaki, na Abednego hawakuiinamia. Watu fulani wakawaona na wakaambia hivi mufalme: ‘Wale Waebrania watatu wamekataa kuabudu sanamu yako.’ Nebukadneza akatuma watu wawaite na akawaambia: ‘Mara hii, kama tu munasikia muziki, muabudu sanamu yenye nilisimamisha. Kama hamuiabudu, nitawatupa ndani ya tanuru ya moto. Hakuna mungu mwenye ataweza kuwaokoa.’ Wakamujibu: ‘Hatutaabudu sanamu yako. Mungu wetu anaweza kutuokoa. Na hata kama hatuokoe, Ee mufalme, ujue kama hatutaabudu sanamu yako.’

Nebukadneza akakasirika sana. Akaambia wanaume wake: ‘Muwashe moto mara saba kuliko kawaida!’ Kisha akaambia maaskari wake: ‘Mufunge hawa wanaume, na muwatupe ndani ya tanuru!’ Wakati wale maaskari walifika karibu na ile tanuru, walikufa palepale juu ilikuwa na moto ya nguvu sana. Wale Waebrania watatu wakaangukia mu ile moto. Lakini Wakati Nebukadneza aliangalia ndani ya tanuru, aliona wanaume ine wako wanatembea mu moto. Akaogopa sana na kuuliza maaskari wake: ‘Tulitupa wanaume tatu ndani ya moto, haiko vile? Sasa ninaona wanaume ine. Na mumoja anafanana malaika!’

Nebukadneza akaenda karibu na mulango wa tanuru na kusema kwa sauti: ‘Watumishi wa Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi, mutoke mu moto!’ Kila mutu alishangaa kuona namna Shadraki, Meshaki, na Abednego wanatoka mu moto bila kuumia hata kidogo. Ngozi yao, nywele zao, na nguo zao hazikuungua. Na hawakunuka harufu ya moto hata kidogo.

Kisha Nebukadneza akasema: ‘Mungu wa Shadraki, Meshaki, na Abednego ni mukubwa. Alituma malaika wake awaokoe. Hakuna mungu sawa Mungu wao.’

Je, umeazimia kubakia muaminifu, sawa wale Waebrania watatu, hata kutokee nini?

“Yehova Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu, na yeye peke yake ndiye unapaswa kutolea utumishi mutakatifu.” ​—Matayo 4:10