Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

62

Ufalme Wenye Uko Sawa Muti Mukubwa

Ufalme Wenye Uko Sawa Muti Mukubwa

Usiku moja, Nebukadneza alilota ndoto ya kuogopesha. Aliita wanaume wake wenye hekima ili wamufasirie maana ya ile ndoto, lakini hakuna mwenye aliweza. Ku mwisho, mufalme alituma watu waite Danieli.

Nebukadneza aliambia Danieli: ‘Mu ndoto yangu, niliona muti. Ile muti ilirefuka mupaka ikafika mbinguni. Watu mu dunia yote wangeweza kuiona. Ilikuwa na majani ya muzuri, na ilikuwa na matunda ya mingi. Wanyama walikuwa wanapumuzika chini ya kivuli cha ule muti, na ndege wa mbinguni walijenga chicha (nyumba zao) ku matawi yake. Kisha malaika alishuka kutoka mbinguni na kusema kwa sauti kubwa: “Mukate muti na matawi yake. Lakini, muache kisiki na mizizi yake mu udongo, na muzungushe ku kile kisiki pingu ya chuma na ya shaba. Moyo wa ile muti, wenye ulikuwa moyo wa mwanadamu, utabadilika na kuwa moyo wa munyama, na utabakia vile nyakati saba. Watu wote watajua kama Mungu njo Mufalme na anaweza kupatia ufalme mutu yeyote mwenye anataka.”’

Yehova alijulisha Danieli maana ya ile ndoto. Wakati Danieli alielewa maana ya ile ndoto, akaogopa sana. Akaambia Nebukadneza: ‘Ee mufalme, ingekuwa muzuri kama hii ndoto ingehusu maadui wako, lakini inakuhusu wewe. Wewe njo ule muti mukubwa wenye ulikatwa. Hautakuwa tena mufalme, na utakula majani sawa munyama wa pori. Lakini, kwa sababu malaika alisema waache kisiki na mizizi yake mu udongo, utakuwa tena mufalme kisha wakati fulani.’

Kisha mwaka moja, Nebukadneza alikuwa anatembea juu ya nyumba yake ya kifalme, na alikuwa anaangalia uzuri wa muji wa Babiloni. Alikuwa anasema: ‘Huu muji wenye nimejenga ni wa muzuri sana. Niko mukubwa sana!’ Wakati alikuwa anasema vile, sauti kutoka mbinguni ikamuambia: ‘Nebukadneza! Hauko tena mufalme.’

Palepale, akili ya Nebukadneza ikaharibika. Akakuwa sawa munyama wa pori. Wakamufukuza mu nyumba yake ya kifalme na akaanza kuishi na wanyama mu pori. Nywele za Nebukadneza zikakuwa murefu sawa manyoya ya tai, na makucha yake ikakuwa sawa makucha ya ndege.

Wakati miaka saba ilipita, akili ya Nebukadneza ikarudia na Yehova akamufanya tena kuwa mufalme wa Babiloni. Kisha Nebukadneza akasema: ‘Ninamusifu Yehova, Mufalme wa mbinguni. Sasa ninajua kama Yehova njo Mufalme. Anashusha wenye kiburi, na anapatia ufalme mutu yeyote mwenye anataka.’

“Kiburi kinatangulia kuanguka, na roho yenye majivuno inatangulia kujikwaa.”​—Mezali 16:18