Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

63

Maneno Inaandikwa Kwenye Ukuta

Maneno Inaandikwa Kwenye Ukuta

Kisha wakati fulani, Belshaza akakuwa mufalme wa Babiloni. Usiku moja, mufalme alialika ku karamu watu elfu moja wa maana sana mu inchi. Wakati wa karamu, aliomba watumishi wake walete vikombe vya zahabu vyenye Nebukadneza alitoshaka mu hekalu la Yehova. Belshaza na wageni wake wakatumia vile vikombe ili kunywa divai na wakasifu miungu yao. Palepale, mukono wa mutu ukatokea na kuanza kuandika maneno yenye haieleweke ku ukuta wa chumba cha kukulia chakula.

Belshaza akaogopa sana. Akaita watu wake wenye kufanya uchawi na kuwaambia: ‘Mwenye ataweza kuniambia maana ya ile maneno, nitamufanya kuwa mutu wa tatu mwenye mamlaka sana mu Babiloni.’ Wakajaribu lakini hakuna mwenye aliweza kueleza maana ya ile maneno. Kisha malkia akakuja na kusema: ‘Kuko mutu mwenye alikuwaka anafasiria Nebukadneza mambo mbalimbali. Jina lake Danieli. Anaweza kukufasiria maana ya hii maneno.’

Wakaleta Danieli mbele ya mufalme. Belshaza akamuambia: ‘Kama unaweza kusoma hii maneno na kuifasiria, nitakupatia mukufu wa zahabu na nitakufanya kuwa mutu wa tatu mwenye mamlaka sana mu inchi ya Babiloni.’ Lakini, Danieli akamuambia: ‘Sitaki zawadi zako. Lakini nitakuambia maana ya hii maneno. Baba yako, Nebukadneza, alikuwaka na kiburi, lakini Yehova alimushusha. Unajua mambo yote yenye ilimupataka. Lakini, umekosea Yehova heshima juu ulitumia vikombe vya hekalu lake ili kunywa divai. Njo maana Mungu ameandika hii maneno: Mene, Mene, Tekeli, na Parsini. Ile maneno inamaanisha kama Wamedi na Waajemi watapata ushindi juu ya Babiloni, na wewe hautakuwa tena mufalme.’

Ilionekana sawa vile hakuna mwenye angeweza kupata ushindi juu ya Babiloni. Ule muji ulikuwa unalindwa na ukuta wenye nguvu na muto murefu sana kuenda chini. Lakini uleule usiku tu, Wamedi na Waajemi wakakuja kupigana na Babiloni. Koreshi, mufalme wa Uajemi, alifanya maji fulani ya muto ipite fasi ingine juu maaskari wake waweze kufika ku milango mikubwa ya Babiloni. Wakati walifika, ile milango ilikuwa wazi! Basi, maaskari wakaingia katika muji, wakapata ushindi juu ya muji, na wakaua mufalme. Kisha Koreshi akakuwa mufalme wa Babiloni.

Mbele ya mwaka moja kuisha, Koreshi alitangaza hivi: ‘Yehova ameniambia nijenge upya hekalu lake kule Yerusalemu. Kila mutu mwenye kuwa kati ya watu wake mwenye anapenda kusaidia ku ile kazi ya kujenga, anaweza kuenda.’ Kwa hiyo, kama vile Yehova alikuwa ametabiri, Wayahudi wengi walirudia kwao miaka 70 kisha Yerusalemu kuharibiwa. Koreshi alirudisha vikombe vya zahabu na feza na vyombo vyenye Nebukadneza alitoshaka mu hekalu. Unaona vile Yehova alitumia Koreshi juu ya kusaidia watu wake?

“Ameanguka! Babiloni Mukubwa ameanguka, na amekuwa makao ya pepo wachafu.”​—Ufunuo 18:2