Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

64

Danieli Anatupwa Ndani ya Shimo la Simba

Danieli Anatupwa Ndani ya Shimo la Simba

Mufalme mwingine wa Babiloni alikuwa Dario Mumedi. Alitambua kama Danieli hakukuwa sawa na watu wengine. Alimuweka Danieli kuwa mukubwa wa watu wake wa maana sana mu inchi. Wale watu walisikilia Danieli wivu na walitaka kumuua. Walijua kama Danieli alizoea kusali kwa Yehova mara tatu kila siku. Basi waliambia Dario: ‘Ee mufalme, inafaa kukuwe sheria yenye kuomba kila mutu akuwe anatoa sala kwako tu. Kama mutu fulani hatii ile sheria anapaswa kutupwa ndani ya shimo la simba.’ Dario alifurahia wazo hilo na akatia sinyatire yake ku ile sheria.

Wakati tu Danieli alipata habari juu ya ile sheria ya mupya, akaenda kwake. Akapiga magoti mbele ya dirisha lake lenye lilikuwa wazi, na akaanza kusali kwa Yehova. Wale wanaume wenye walikuwa wanamusikilia Danieli wivu waliingia mu nyumba yake na kumukuta iko anasali. Mara moja wakaenda haraka kwa Dario na kumuambia: ‘Danieli hatii sheria yako. Iko anasali kwa Mungu wake mara tatu kila siku.’ Dario alikuwa anamupenda Danieli, na hakupenda akufe. Siku muzima alikuwa anawaza atafanya nini ili kumuokoa Danieli. Lakini hata mufalme hakukuwa na ruhusa ya kubadilisha sheria yenye yeye mwenyewe alikuwa ametia sinyatire. Dario alilazimika kupatia watu wake amri ya kutupa Danieli ndani ya shimo mwenye mulikuwa simba wakali.

Ule usiku, Dario alikuwa na wasiwasi sana juu ya Danieli na hakuweza kulala usingizi. Asubui, alienda mbio kwenye shimo la simba na kuuliza Danieli: ‘Mungu wako alikuokoa?’

Dario akasikia sauti. Ilikuwa sauti ya Danieli! Danieli akamujibu Dario: ‘Malaika wa Yehova alifunga vinywa vya simba. Hawakuniumiza hata kidogo.’ Dario alifurahi sana! Akatoa amri watoshe Danieli ndani ya ile shimo. Simba hawakumuumiza Danieli hata kidogo. Kisha mufalme akatoa amri hii: ‘Mutupe ndani ya shimo la simba wanaume wenye walimushitaki Danieli.’ Wakati walitupa wale wanaume ndani ya shimo, mara moja simba wakawakula.

Dario alitumia watu wake wote amri hii: ‘Kila mutu anapaswa kuogopa Mungu wa Danieli juu alimuokoa Danieli ndani ya shimo la simba.’

Na wewe, unazoea kusali kwa Yehova kila siku kama Danieli?

“Yehova anajua namna ya kukomboa kutoka katika jaribu watu wenye ushikamanifu kwa Mungu.”​—2 Petro 2:9