Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

65

Esta Anaokoa Watu Wake

Esta Anaokoa Watu Wake

Esta alikuwa mwanamuke Muyahudi mwenye aliishi katika muji wa Shushani, wenye ulikuwa katika eneo la Uajemi. Zamani, familia yake ilikuwaka inaishi Yerusalemu, lakini Nebukadneza aliwachukua na kuwapeleka Babiloni. Mordekai, mutoto wa ndugu ya baba yake, njo alimukomalishaka. Na Mordekai alikuwa mutumishi wa Mufalme Ahasuero wa Uajemi.

Mufalme Ahasuero alipenda akuwe na malkia mupya. Watumishi wake walimuletea wanamuke wenye walikuwa na sura ya muzuri sana mu inchi, na Esta alikuwa kati yao. Kati ya wale wanamuke wote, mufalme alichagua Esta akuwe malkia. Mordekai aliambia Esta asijulishe watu kama yeye ni Muyahudi.

Mwanaume mumoja mwenye kuitwa Hamani njo alikuwa mukubwa wa wakubwa wote, na alikuwa na kiburi. Alitaka kila mutu amuinamie. Mordekai alikataa kumuinamia. Na Hamani alikasirika sana na alitafuta kumuua. Wakati Hamani alivumbua kama Mordekai alikuwa Muyahudi, alifanya mupango wa kuua Wayahudi wote mu ile inchi. Aliambia mufalme: ‘Wayahudi ni watu wabaya; unapaswa kuwaua wote.’ Ahasuero akasema: ‘Fanya vile unapenda.’ Kisha akamuruhusu atunge sheria ya mupya. Hamani akatunga sheria yenye iliomba watu waue Wayahudi wote siku ya 13 ya mwezi wa Adari. Lakini Yehova alikuwa anaona ile mambo yote.

Esta hakujua kama ile sheria ilikuwa imetungwa. Kwa hiyo, Mordekai alimutumia kopi ya ile sheria na kumuambia: ‘Uende uzungumuze na mufalme.’ Esta akasema: ‘Kama mutu anaenda kumuona mufalme bila kuitwa watamuua. Sasa, kumepita siku 30 na mufalme hajaniita! Lakini nitaenda. Kama ananinyooshea fimbo yake ya ufalme, nitaishi. Kama hafanye vile, wataniua.’

Esta akaingia mu kiwanja cha nyumba ya mufalme. Wakati mufalme alimuona, akamunyooshea fimbo yake ya ufalme. Mara moja Esta akaenda karibu na mufalme, na mufalme akamuuliza: ‘Esta, unataka nini?’ Akasema: ‘Ninapenda wewe na Hamani mufike kwenye karamu yangu.’ Wakati walikuwa ku ile karamu, Esta akawaambia wafike tena ku karamu ya pili. Wakati walikuwa ku karamu ya pili, mufalme akauliza tena: ‘Unataka nini?’ Akasema: ‘Kuko mutu mwenye anataka kuniua, mimi na watu wangu. Tafazali, utuokoe.’ Mufalme akauliza: ‘Ni nani njo anataka kukuua?’ Esta akajibu: ‘Ni huyu Hamani, mutu mubaya.’ Ahasuero akakasirika sana na kusema waue Hamani siku ileile.

Lakini hakuna mutu mwenye angeweza kubadilisha sheria yenye Hamani alikuwa ametunga, hata mufalme hangeweza. Kwa hiyo, mufalme akafanya Mordekai kuwa mukubwa wa wakubwa wote na akamupatia mamlaka ya kutunga sheria ya mupya. Mordekai akatunga sheria yenye iliruhusu Wayahudi wapigane kama maadui wao wanakuja kupigana nao. Mu siku ya 13 ya mwezi wa Adari, Wayahudi walipata ushindi juu ya maadui wao. Tangu ile siku, Wayahudi walianza kukumbuka ule ushindi kila mwaka.

“Mutapelekwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwatolea wao na mataifa ushahidi.”​—Matayo 10:18