Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

66

Ezra Alifundisha Watu Sheria ya Mungu

Ezra Alifundisha Watu Sheria ya Mungu

Miaka 70 hivi ilikuwa imepita tangu Waisraeli warudie Yerusalemu, lakini wamoja kati yao walikuwa wangali wanaishi mu maeneo mbalimbali ya utawala wa Uajemi. Mumoja wao alikuwa kuhani mwenye aliitwa Ezra, mwenye alikuwa anafundisha watu Sheria ya Yehova. Ezra alisikia kama wakaaji wa Yerusalemu hawakukuwa wanafuata Sheria ya Yehova. Kwa hiyo, alipenda kuenda kule ili awasaidie. Mufalme Artashasta wa Uajemi alimuambia: ‘Mungu alikufanya ukuwe na hekima ili ufundishe watu Sheria yake. Unaweza kuenda Yerusalemu, wewe na kila mutu mwenye atapenda kuenda pamoja na wewe.’ Kwa hiyo, Ezra na wote wenye walipenda kurudia Yerusalemu wakaenda. Mbele waende, walimuomba Yehova awalinde katika safari yao ya murefu.

Kisha miezi ine, wakafika Yerusalemu. Kisha wakubwa wenye walikuwa Yerusalemu wakaambia Ezra hivi: ‘Waisraeli wamekataa kumutii Yehova: wameoa wanamuke wenye kuabudu miungu ya uongo.’ Ezra alifanya nini? Ezra alipiga magoti mbele ya watu na kusali hivi: ‘Yehova, umetufanyia mambo mingi sana! Lakini, sisi tumekutendea zambi.’ Wakaaji wa Yerusalemu walitubu, lakini waliendelea kufanya mambo yenye haikukuwa sawa. Kwa hiyo, Ezra alichagua wazee na waamuzi ili washugulikie tatizo hilo. Katika miezi tatu yenye ilifuata, walifukuza wale wenye hawakukuwa wanamuabudu Yehova.

Miaka 12 ikapita. Katika kile kipindi cha wakati, kuta za Yerusalemu zilijengwa upya. Kwa hiyo Ezra alikusanya watu katika kiwanja cha watu wote ili awasomee Sheria ya Mungu. Wakati Ezra alifungua kitabu cha Sheria, watu wakasimama. Kisha akamusifu Yehova, na watu wakainua mikono ili kuonyesha kama wanakubali mambo yenye anasema. Kisha Ezra alisoma na kufasiria Sheria, na watu walisikiliza sana. Walikubali kama walikuwa wamemukosea tena Yehova, na wakalia. Siku yenye ilifuata, Ezra aliendelea kuwasomea Sheria. Walitambua kama karibuni walipaswa kufanya Sikukuu ya Vibanda. Mara moja, wakaanza kujitayarisha kwa ajili ya ile sikukuu.

Kwa siku saba za sikukuu, watu walifurahi sana na walimushukuru Yehova juu ya mavuno ya muzuri yenye walipata. Walikuwa hawajafanyaka Sikukuu ya Vibanda ya namna ile tangu siku za Yoshua. Kisha ile sikukuu, watu walikusanyika na kusali hivi: ‘Yehova, ulitutosha katika utumwa, ulitukulisha katika jangwa, na kutupatia hii inchi yenye kupendeza. Lakini mara mingi, tulikosa kukutii. Ulitutumia manabii ili watuonye, lakini hatukuwasikiliza. Lakini, ulituvumilia. Ulitimiza ahadi yenye ulitolea Abrahamu. Sasa tunatoa ahadi kama tutakutii.’ Halafu wakaandika ahadi yao, na wakubwa, Walawi, na makuhani wakatia muhuri juu yake.

“Wenye furaha ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulishika!”​—Luka 11:28