Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

68

Elizabeti Anakuwa na Mutoto

Elizabeti Anakuwa na Mutoto

Wakati kulikuwa kumepita miaka zaidi ya 400 tangu kazi ya kujenga upya kuta za Yerusalemu imalizike, kuhani mwenye Aliitwa Zekaria na bibi yake Elizabeti, walikuwa wanaishi karibu na Yerusalemu. Walikuwa wamefanya miaka mingi mu ndoa, lakini hawakukuwa na watoto. Siku moja, wakati Zekaria alikuwa anachoma uvumba katika patakatifu pa hekalu, malaika Gabrieli alimutokea. Zekaria aliogopa sana, lakini Gabrieli alimuambia: ‘Usiogope. Ninakuletea habari ya muzuri yenye inatoka kwa Yehova. Bibi yako, Elizabeti, atazaa mutoto na jina lake litakuwa Yohana. Yehova amechagua Yohana kwa ajili ya kazi fulani ya pekee.’ Zekaria akamuuliza: ‘Nitajua namna gani kama unasema kweli? Mimi na bibi yangu tumezeeka, hatuwezi kuzaa mutoto.’ Gabrieli akamuambia: ‘Mungu njo alinituma nikuambie hii habari. Sasa, kwa sababu hauniamini, utakuwa bubu mupaka wakati ule mutoto atazaliwa.’

Zekaria alikawia sana katika patakatifu. Wakati alitoka inje, watu wenye walikuwa wanamungoja walipenda kujua kama kulitokea nini. Lakini Zekaria akashindwa kusema. Alifanya tu alama kwa kutumia mikono yake. Wakati watu waliona vile, walitambua kama Zekaria alikuwa amepata ujumbe kutoka kwa Mungu.

Kisha, Elizabeti akakuwa na mimba na akazaa mutoto mwanaume, kama vile malaika alikuwa amesema. Marafiki na watu wa jamaa yake walikuja kuona mutoto. Walifurahi sana. Elizabeti aliwaambia: ‘Jina lake litakuwa Yohana.’ Wakamuambia: ‘Hakuna mutu wa jamaa yako mwenye anaitwa kwa jina hilo. Umupatie jina Zekaria, jina la baba yake.’ Lakini Zekaria akaandika hii maneno: ‘Jina lake Yohana.’ Palepale, Zekaria akaanza tena kusema! Habari ya ule mutoto ikaenea fasi yote mu muji wa Yudea. Watu walishangaa sana na walikuwa wanajiuliza: ‘Huyu mutoto atakuwaka nani?’

Kisha Zekaria akajazwa roho takatifu, na akatoa unabii huu: ‘Yehova asifiwe. Alitoa ahadi kwa Abrahamu kama atatuma Masiya ili atuokoe. Yohana atakuwa nabii na atatayarisha njia kwa ajili ya kuja kwa Masiya.’

Jambo fulani la pekee lilifikia pia Maria, mutu wa jamaa ya Elizabeti. Tutaona jambo hilo mu sura yenye kufuata.

“Kwa wanadamu jambo hilo haliwezekane, lakini kwa Mungu mambo yote yanawezekana.”​—Matayo 19:26