Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

69

Gabrieli Anatembelea Maria

Gabrieli Anatembelea Maria

Katika jamaa ya Elizabeti, mulikuwa kijana mwanamuke mwenye aliitwa Maria. Maria alikuwa anaishi katika muji wa Nazareti, kule Galilaya. Alikuwa muchumba wa seremala mwenye aliitwa Yosefu. Wakati Elizabeti alikuwa na mimba ya miezi sita, malaika Gabrieli alimutokea Maria na akamuambia hivi: ‘Jambo, Maria. Yehova amekupendelea sana.’ Maria hakuelewa Gabrieli alipenda kusema nini. Kisha Gabrieli akamuambia: ‘Utapata mimba na utazaa mutoto. Utamuita Yesu. Atakuwa Mufalme na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.’

Maria akamuambia: ‘Lakini mimi sijalalaka na mwanaume. Namna gani nitazaa mutoto?’ Gabrieli akamuambia: ‘Kwa Yehova hakuna jambo lenye haliwezekane. Roho takatifu itakuja juu yako, na utazaa mutoto mwanaume. Elizabeti, mutu wa jamaa yako, naye amekuwa na mimba.’ Kisha Maria akasema: ‘Niko mutumwa wa Yehova. Ikuwe vile unasema.’

Kisha, Maria akaenda kuona Elizabeti. Elizabeti alikuwa anaishi katika muji fulani wenye ulikuwa ku milima. Wakati Maria alimusalimia, mara moja Elizabeti akasikia mutoto mwenye alikuwa mu tumbo lake anaruka. Akajazwa roho takatifu na akasema: ‘Maria, Yehova amekubariki. Nimepata pendeleo kubwa sana kwa sababu mama ya Masiya amefika katika nyumba yangu.’ Maria akajibu: ‘Ninamusifu Yehova kwa moyo wangu wote.’ Maria akabakia miezi tatu kwa Elizabeti, kisha akarudia Nazareti, kwenye alikuwa anaishi.

Wakati Yosefu alipata habari kama Maria alikuwa na mimba, alipenda waachane. Lakini malaika akamutokea mu ndoto na kumuambia: ‘Usiogope kumuoa. Hakufanya kosa hata kidogo.’ Basi, Yosefu akaoa Maria na akamupeleka mu nyumba yake.

“Yehova anafanya kila kitu chenye anapenda kufanya katika mbingu na juu ya dunia.”​—Zaburi 135:6