Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

70

Malaika Wanatangaza Kama Yesu Amezaliwa

Malaika Wanatangaza Kama Yesu Amezaliwa

Mutawala wa Roma, Kaisari Augusto, alitoa amri kama Wayahudi wote waende kujiandikisha mu miji yao. Kwa hiyo, Yosefu na Maria walirudia Betlehemu, kwenye familia ya Yosefu ilitokaka. Wakati huo, Maria alikuwa karibu kuzaa.

Wakati walifika Betlehemu, walikosa fasi ya muzuri ya kubakia. Kwa hiyo, walienda kukaa fasi ya kulalishia wanyama. Mule njo Maria alizalia mutoto wake, Yesu. Alimufunga na vitambaa laini na kumulalisha mu chombo cha kukulishia wanyama.

Karibu na Betlehemu, kulikuwa wachungaji fulani wenye walikuwa inje usiku. Walikuwa wanachunga makundi yao ya wanyama. Palepale, malaika akasimama pembeni yao na mwangaza wa utukufu wa Yehova ukaangaza pande zote. Wachungaji wakaogopa, lakini malaika akawaambia: ‘Musiogope, niko na habari ya muzuri sana ya kuwaambia. Leo, Masiya amezaliwa Betlehemu.’ Mara moja, malaika wengi wakajiunga na ule malaika, na kusema: ‘Utukufu kwa Mungu kule juu, na amani ku dunia.’ Kisha wale malaika hawakuonekana tena. Sasa, wachungaji walifanya nini?

Wachungaji wakaambiana hivi: ‘Tuende mara moja Betlehemu.’ Wakaenda haraka na wakakuta Yosefu na Maria na mutoto wao mudogo fasi ya kulalishia wanyama.

Wote wenye walisikia mambo yenye malaika aliambia wachungaji walishangaa sana. Maria alifikiri sana kuhusu maneno ya ule malaika na hakuisahau hata kidogo. Basi wachungaji wakarudia kuchunga makundi yao ya wanyama na wakamushukuru Yehova juu ya mambo yote yenye waliona na kusikia.

“Nilitoka kwa Mungu na niko hapa. Sikukuja kwa uamuzi wangu mwenyewe, lakini Yeye ndiye alinituma.”​—Yohana 8:42