Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

71

Yehova Alimulinda Yesu

Yehova Alimulinda Yesu

Mu inchi fulani yenye ilikuwa upande wa mashariki wa Israeli, kulikuwa watu wenye walikuwa wanaamini kama nyota zinaweza kuwaongoza. Usiku moja, wanaume fulani wa kutoka Mashariki waliona kitu cha kufanana na nyota. Ile “nyota” ilikuwa inangaa na ilikuwa inatembea mu anga. Waliifuata na ikawapeleka Yerusalemu. Wakati walifika kule, walianza kuuliza watu hivi: ‘Mutoto mwenye atakuwa mufalme wa Wayahudi iko wapi? Tumekuja kumuinamia.’

Wakati Herode, mufalme wa Yerusalemu, alisikia habari kuhusu ule mufalme wa mupya, akaogopa sana. Akauliza wakubwa wa makuhani: ‘Ule mufalme anapaswa kuzaliwa wapi?’ Wakamuambia: ‘Manabii walisema kama angezaliwa Betlehemu.’ Basi Herode akaita wale wanaume wa kutoka Mashariki na kuwaambia: ‘Muende Betlehemu na mutafute ule mutoto. Kisha, mukuje muniambie kwenye iko. Na mimi ninapenda niende kumuinamia.’ Lakini Herode alikuwa anasema uongo.

Kisha ile “nyota” ikatoka Yerusalemu, na wale wanaume wakaifuata mupaka Betlehemu. Wakati ilifika Betlehemu, ikasimama juu ya nyumba fulani. Kisha, wale wanaume wakaingia mu ile nyumba na wakakuta Yesu na mama yake, Maria. Wakainamia ule mutoto na kumupatia zawadi za zahabu, ubani, na manemane. Unawaza Yehova njo alitumaka wale wanaume watafute Yesu? Hapana.

Ule usiku, Yehova alizungumuza na Yosefu mu ndoto. Alimuambia hivi: ‘Herode anataka kuua Yesu. Ukimbilie Misri, wewe na bibi yako na mutoto wako. Mubakie kule mupaka wakati nitawaambia murudie.’ Palepale, Yosefu na familia yake wakaenda Misri.

Yehova aliambia wale wanaume wa kutoka Mashariki wasirudie kwa Herode. Wakati Herode alivumbua kama wale wanaume walienda bila kupita kwake, alikasirika sana. Kwa sababu hakujua kwenye Yesu alikuwa, akatoa amri ya kusema waue watoto wote wanaume wenye walikuwa na miaka moja na Yesu. Lakini Yesu alikuwa mbali, alikuwa anaishi Misri kwa usalama.

Kisha wakati fulani, Herode alikufa. Kwa hiyo, Yehova aliambia Yosefu: ‘Sasa, hakuna tena hatari munaweza kurudia.’ Yosefu, Maria, na Yesu wakarudia Israeli, na wakaanza kuishi katika muji wa Nazareti.

“Ni vile neno langu lenye kutoka katika kinywa changu litakuwa . . . , na hakika litafanikiwa katika mambo yenye nimelituma kufanya.” ​—Isaya 55:11