Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

72

Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12

Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12

Yosefu na Maria walikuwa wanaishi pamoja na Yesu, na watoto wao wengine wanamuke na wanaume. Ili familia yake ipate namna ya kuishi, Yosefu alikuwa anafanya kazi ya useremala (kazi ya mbao). Na alikuwa anafundisha watu wa familia yake juu ya Yehova na juu ya Sheria ya Yehova. Walizoea kuenda pamoja ku sinagogi juu ya kumuabudu Mungu. Na kila mwaka, walikuwa wanafanya safari ya murefu ya kuenda Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka.

Wakati Yesu alikuwa na miaka 12, familia yao ilienda Yerusalemu, kama vile walizoea kufanya. Yerusalemu ilikuwa imejaa watu wenye walikuja kwa ajili ya Pasaka. Kisha Pasaka, Yosefu na Maria walianza safari ya kurudia ku nyumba. Waliwaza kama Yesu iko na watu wengine wenye walikuwa wanasafiri pamoja nao. Lakini, wakati walimutafuta kati ya watu wa jamaa yao, hawakumupata.

Kwa hiyo, walirudia Yerusalemu na kutafuta Yesu kwa siku tatu. Ku mwisho, walienda ku hekalu. Na walimukuta kule. Alikuwa amekaa katikati ya walimu, alikuwa anawasikiliza sana, na kuwauliza maulizo. Wale walimu walifurahia sana namna Yesu alikuwa anazungumuza na walianza kumuuliza maulizo. Na majibu yake iliwashangaza. Ilionyesha kama alikuwa anaelewa muzuri Sheria ya Yehova.

Yosefu na Maria walikuwa na wasiwasi sana. Wakati Maria aliona Yesu, alisema hivi: ‘Mutoto wangu, tulikutafuta fasi yote! Ulikuwa wapi?’ Yesu akajibu: ‘Hamukujua kama ninapaswa kuwa mu nyumba ya Baba yangu?’

Kisha Yesu akarudia Nazareti pamoja na wazazi wake. Yosefu alifundisha Yesu kazi ya useremala. Unawaza Yesu alikuwa mutu wa namna gani wakati alikuwa kijana? Wakati aliendelea kukomaa, Yesu aliendelea kuwa na hekima. Mungu na watu waliendelea kumufurahia zaidi na zaidi.

“Ee Mungu wangu, ninafurahia kufanya mapenzi yako, na sheria yako iko ndani yangu kabisa.”​—Zaburi 40:8