Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

73

Yohana Anatayarisha Kuja kwa Masiya

Yohana Anatayarisha Kuja kwa Masiya

Wakati alikomaa, Yohana, mutoto wa Zekaria na Elizabeti, akakuwa nabii. Yehova alipatia Yohana kazi ya kufundisha watu kama Masiya alikuwa karibu kuja. Lakini kuliko kufundisha mu masinagogi ao mu miji, Yohana alihubiri mu jangwa. Wakaaji wa Yerusalemu na Yudea yote walikuwa wanaenda kumuona ili awafundishe. Na alifundisha kama walipaswa kuacha mambo ya mubaya ili wamufurahishe Mungu. Kisha kumusikiliza, wengi walitubu zambi zao, na Yohana aliwabatiza katika Muto Yordani.

Yohana alikuwa anaishi maisha ya mwepesi. Alikuwa anavaa nguo ya manyoya ya ngamia na alikuwa anakula nzige na asali ya pori. Watu walikuwa wanapenda kujua mambo mingi juu ya Yohana. Hata Wafarisayo na Wasadukayo, wenye walikuwa na kiburi, walienda kumuona. Yohana aliwaambia: ‘Munapaswa kubadilika na kutubu. Musiwaze kama muko wa maana kupita watu wengine. Munasema kama muko watoto wa Abrahamu, lakini ile haimaanishe kama muko watoto wa Mungu.’

Watu mingi walikuja kumuona Yohana. Walimuuliza: ‘Tunapaswa kufanya nini ili tufurahishe Mungu?’ Yohana aliwaambia: ‘Kama uko na nguo mbili, moja uipatie mwenye hana.’ Unajua juu ya nini alisema vile? Alipenda watu wajue kama, ili wamufurahishe Mungu, iliomba wapende wengine.

Yohana aliwaambia wakusanya-kodi: ‘Mukuwe wanyoofu na musikuwe munadanganya watu.’ Aliambia maaskari: ‘Musikamate rushwa (kata-midomo) na musiseme uongo.’

Makuhani na Walawi pia walienda kuona Yohana. Walimuuliza: ‘Uko nani? Tunapenda kujua.’ Yohana akawaambia: ‘Mimi ni sauti yenye iko inasema mu jangwa. Niko ninapeleka watu kwa Yehova, sawa vile Isaya alisemaka.’

Watu walipenda sana mambo yenye Yohana alikuwa anawafundisha. Wengi walijiuliza ikiwa Yohana alikuwa Masiya. Lakini aliwaambia: ‘Mutu fulani mwenye kuwa mukubwa kunipita iko anakuja. Sistahili hata kumuvua viato. Mimi niko ninabatiza kwa maji, lakini yeye, atabatiza kwa roho takatifu.’

“Mutu huyo alikuja kama shahidi, ili atoe ushahidi juu ya mwangaza, kusudi watu wa namna zote waamini kupitia yeye.”​—Yohana 1:7