Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

75

Ibilisi Anamujaribu Yesu

Ibilisi Anamujaribu Yesu

Kisha Yesu kubatizwa, roho takatifu ilimuongoza aende mu jangwa. Alifanya kule siku 40, bila kula. Kisha alisikia njaa sana. Halafu Ibilisi akakuja ili amujaribu. Akamuambia: ‘Kama uko Mutoto wa Mungu, ambia hii majiwe ikuwe mikate.’ Lakini Yesu akamujibu kwa kutaja Maandiko. Akamuambia: ‘Imeandikwa kama, ili mutu aishi, hana lazima ya chakula peke yake. Anapaswa pia kusikiliza kila neno lenye Yehova anasema.’

Kisha, Ibilisi akamujaribu mara ya pili. Akamuambia: ‘Kama uko kabisa Mutoto wa Mungu, ujitupe chini kutoka kwenye sehemu ya juu sana ya hekalu. Imeandikwa kama Mungu atatuma malaika zake juu wakubebe katika mikono yao.’ Lakini Yesu akajibu tena kwa kutaja Maandiko. Akasema: ‘Imeandikwa kama haupaswe kumujaribu Yehova.’

Kisha, Shetani akamuonyesha Yesu falme zote za dunia, na utajiri na utukufu wa zile falme. Halafu akamuambia Yesu: ‘Nitakupatia hizi falme zote na utukufu wazo kama unaniabudu mara moja tu.’ Lakini Yesu akamujibu: ‘Toka mbele yangu, Shetani! Imeandikwa kama Yehova tu njo unapaswa kuabudu.’

Kisha, Ibilisi akamuacha, na malaika wakakuja na kumupatia Yesu chakula. Kuanzia wakati huo, Yesu akaanza kuhubiri habari njema ya Ufalme. Njo kazi yenye Mungu alimutumaka akuje kufanya ku dunia. Watu walipenda sana mambo yenye Yesu aliwafundisha, na walikuwa wanamufuata fasi yote kwenye alikuwa anaenda.

“Wakati [Ibilisi] anasema uongo, anasema kulingana na muelekeo wake mwenyewe, kwa sababu yeye ni muongo na baba ya uongo.” ​—Yohana 8:44