Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 76

Yesu Analisafisha Hekalu

Yesu Analisafisha Hekalu

Katika mwaka wa 30 W.K., Yesu alienda Yerusalemu. Watu wengi walikuwa wameenda jijini humo kusherehekea Pasaka. Sherehe hiyo ilitia ndani kudhabihu wanyama hekaluni. Watu fulani walikuja na wanyama wao, lakini wengine waliwanunua huko Yerusalemu.

Yesu alipoenda hekaluni, aliwaona watu wakiuza wanyama ndani ya hekalu. Walikuwa wakijipatia pesa ndani ya nyumba ya Yehova ya ibada! Yesu alitendaje? Alitengeneza mjeledi wa kamba naye akawafukuza kondoo na ng’ombe kutoka hekaluni. Akapindua meza za watu waliokuwa wakibadili pesa na kumwaga sarafu zao chini. Yesu akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa: ‘Ondoeni vitu hivi kutoka hapa! Acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!’

Watu waliokuwa hekaluni walishangazwa na jambo ambalo Yesu alifanya. Wanafunzi wake wakakumbuka unabii huu uliomhusu Masihi: ‘Nitakuwa na bidii nyingi kwa ajili ya nyumba ya Yehova.’

Baadaye, katika mwaka wa 33 W.K., Yesu alisafisha hekalu kwa mara ya pili. Hangemruhusu mtu yeyote aishushie heshima nyumba ya Baba yake.

“Hamwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Mali.”​—Luka 16:13