Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

79

Yesu Anafanya Miujiza Mingi

Yesu Anafanya Miujiza Mingi

Yesu alikuja ku dunia ili atangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu. Lakini Yehova alimupatia pia roho takatifu ili afanye miujiza. Ile miujiza ilionyesha mambo yenye atafanya wakati atakuwa Mufalme. Yesu alikuwa anaponyesha kila ugonjwa. Kila nafasi kwenye alienda, wagonjwa walikuja kumuona, na aliwaponyesha wote. Vipofu waliona, viziwi walisikia, vilema walitembea, na wale wenye walikuwa na pepo wachafu hawakusumbuliwa nao tena. Watu walipona hata wakati waligusa tu sehemu ya chini ya nguo ya Yesu. Watu walimufuata Yesu kila nafasi kwenye alienda. Hata wakati alipenda kuwa peke yake, Yesu hakufukuza mutu mwenye alienda kumuona.

Siku moja, wakati Yesu alikuwa mu nyumba fulani, watu walimuletea mwanaume mwenye alikuwa amepooza. Lakini hawakuweza kumuingiza mu ile nyumba kwa sababu mulikuwa watu mingi. Kwa hiyo, walitoboa tundu ku sehemu ya juu ya ile nyumba na kushusha ule mwanaume mupaka kwenye Yesu alikuwa. Kisha Yesu aliambia ule mwanaume: ‘Simama utembee.’ Wakati alisimama na kutembea, watu walishangaa sana!

Siku ingine, wakati Yesu alikuwa anaingia mu kijiji fulani, wanaume kumi wenye walikuwa na ugonjwa wa ukoma walisimama mbali na kulalamika: ‘Yesu, utusaidie!’ Katika zile siku, watu wenye walikuwa na ugonjwa wa ukoma hawakuruhusiwa kuwakaribia watu wengine. Yesu aliambia wale wanaume waende ku hekalu, kwa sababu Sheria ya Yehova ilisema kama watu wenye walikuwa na ugonjwa wa ukoma walipaswa kuenda ku hekalu kisha wao kuponyeshwa. Wakati walikuwa mu njia, walipona. Wakati mumoja wao alitambua kama ameponyeshwa, alirudia kuambia Yesu aksanti na kumusifu Mungu. Ni ule mumoja tu njo alimushukuru Yesu.

Kulikuwa mwanamuke mumoja mwenye alikuwa amefanya miaka 12 na iko mugonjwa. Alipenda sana apone. Kwa hiyo, alikuja nyuma ya Yesu katikati ya watu mingi na kugusa sehemu ya chini ya nguo ya Yesu. Na palepale, akapona. Kisha Yesu akauliza: “Nani alinigusa?” Hata kama ule mwanamuke aliogopa sana, alienda karibu na Yesu na kumuambia kweli yote. Yesu alimutuliza kwa kumuambia: ‘Binti yangu, uende kwa amani.’

Ofisa mumoja mwenye jina lake lilikuwa Yairo alimulilia Yesu hivi: ‘Kuja kwangu! Mutoto wangu mwanamuke ni mugonjwa sana.’ Lakini ule mutoto alikufa mbele Yesu afike kwa Yairo. Wakati Yesu alifika, alikuta watu mingi wako wanalia pamoja na ile familia. Yesu akawaambia: ‘Musilie; huyu mutoto analala tu.’ Kisha akamukamata ku mukono na kusema: “Mutoto, amuka!” Palepale akasimama, na Yesu akaambia wazazi wake wamupatie chakula. Unawaza wazazi wake walijisikia namna gani?

“Mungu alimutia mafuta kwa roho takatifu na nguvu, na akapita katika inchi akitenda mema na kuponyesha wote wenye walikandamizwa na Ibilisi, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.”​—Matendo 10:38