Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

81

Mahubiri Kwenye Mulima

Mahubiri Kwenye Mulima

Kisha kuchagua mitume 12, Yesu alitoka ku mulima na kushuka mupaka fasi kwenye watu mingi walikuwa wamekusanyika. Wale watu walitoka Galilaya, Yudea, Tiro, Sidoni, Siria, na ngambo ingine ya Yordani. Walimuletea wagonjwa na watu wenye walikuwa wanateswa na pepo wachafu. Yesu aliwaponyesha wote. Kisha akakaa juu kidogo ku mulima, na akaanza kusema. Alionyesha mambo yenye tunapaswa kufanya ili tukuwe marafiki wa Mungu. Alisema kama tunapaswa kujua kama tuko na lazima ya Yehova na tunapaswa kumupenda. Lakini hatuwezi kumupenda Mungu kama hatupendi kwanza wanadamu wenzetu. Tunapaswa kufanyia kila mutu, hata maadui wetu, mambo ya muzuri na ya haki.

Yesu alisema: ‘Haupaswe kupenda marafiki wako tu. Unapaswa pia kupenda maadui wako na kusamehe wengine kwa moyo wote. Ikiwa unatambua kama mutu fulani amekukasirikia, uende haraka kumuomba musamaha. Ufanyie wengine mambo yenye unapenda wakufanyie.’

Yesu alitoa pia mashauri ya muzuri juu ya vitu vya kimwili. Alisema: ‘Ni muzuri zaidi kuwa rafiki ya Yehova kuliko kuwa na feza mingi. Mwizi anaweza kuiba feza zako, lakini hakuna mwenye anaweza kuiba urafiki wako na Yehova. Musihangaike juu ya kile mutakula, kile mutakunywa, ao kile mutavaa. Muangalie ndege. Hawakosake chakula, kwa sababu Mungu anawahangaikiaka. Kuhangaika hakuwezi kuongeza hata siku moja ku maisha yako. Usisahau kama Yehova anajua mahitaji yako.’

Watu walikuwa hawajasikiaka mutu mwenye alikuwa anazungumuza sawa Yesu. Viongozi wao wa dini hawakukuwa wanawafundisha ile mambo. Juu ya nini Yesu alikuwa mwalimu muzuri vile? Kwa sababu mambo yote yenye alifundisha ilitoka kwa Yehova.

“Mubebe nira yangu na mujifunze kupitia mimi, kwa maana mimi ni mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo, na mutapata pumuziko kwa ajili yenu.”​—Matayo 11:29