Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

82

Yesu Anafundisha Wanafunzi Wake Namna ya Kusali

Yesu Anafundisha Wanafunzi Wake Namna ya Kusali

Mambo yote yenye Wafarisayo walikuwa wanafanya, ilikuwa juu tu ya kujionyesha. Kwa mufano, walikuwa wanatendea wengine mambo ya muzuri juu tu ya kujionyesha. Walikuwa wanasali nafasi za watu mingi juu kila mutu awaone. Walikuwa wanaweka mu akili sala za murefu na walikuwa wanazirudilia-rudilia wakati walikuwa wanasali katika masinagogi ao pembeni ya barabara ili watu wawasikie. Kwa hiyo, watu walishangaa wakati Yesu aliwaambia: ‘Musisali sawa vile Wafarisayo. Wanawazaka kama maneno yenye wanasema itamushangaza Mungu, lakini haimushangazake. Haupaswe kusali ili watu wakuone, sala ni mazungumuzo kati yako na Yehova. Usiseme mambo ileile tena na tena. Yehova anapenda umuambie mambo yenye iko kabisa mu moyo wako.’

“Munapaswa kusali hivi: ‘Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe. Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.’” Yesu aliwaambia tena kama wanapaswa kusali ili wapate chakula kwa ajili ya siku, ili kuomba musamaha wa makosa yao, na wanapaswa kusali juu ya mambo ingine ya kipekee.

Yesu aliongeza: ‘Musiache kusali hata kidogo. Muendelee kumuomba Baba yenu, Yehova, mambo ya muzuri. Kila muzazi anapendaka kupatia mutoto wake vitu vya muzuri. Kama mutoto wako anakuomba mukate, utamupatia jiwe? Kama anaomba samaki, utamupatia nyoka?’

Kisha, Yesu alifasiria mambo yenye ile mufano inatufundisha: ‘Kama ninyi munajua kupatia watoto wenu zawadi za muzuri, munawaza Baba yenu, Yehova, hatawapatia roho takatifu wale wenye kumuomba? Muendelee tu kuomba.’ Na wewe unafuataka shauri hilo la Yesu? Unazoea kusali kwa ajili ya mambo gani?

“Muendelee kuomba, na mutapewa; muendelee kutafuta, na mutapata; muendelee kupiga hodi, na watawafungulia.” ​—Matayo 7:7