Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

84

Yesu Anatembea Juu ya Maji

Yesu Anatembea Juu ya Maji

Yesu alikuwa anaponyesha wagonjwa na kufufua wafu. Lakini alikuwa pia na uwezo wa kutuliza upepo na mvua. Kisha kusali ku mulima, Yesu aliangalia chini na akaona zoruba ku Bahari ya Galilaya. Mitume wake walikuwa mu mashua na walishindwa kuiongoza kwa sababu kulikuwa upepo mukubwa. Yesu alitoka ku mulima na kuanza kutembea juu ya maji na kuja kwenye mashua ilikuwa. Wakati mitume waliona mutu fulani iko anatembea juu ya maji, waliogopa sana. Lakini Yesu aliwaambia: ‘Ni mimi, musiogope.’

Petro akasema: ‘Bwana, kama kweli ni wewe, uniambie nikuje kwenye uko.’ Yesu akamuambia Petro: ‘Kuja.’ Kwa hiyo, wakati zoruba ilikuwa inaendelea, Petro akatoka mu mashua na kuanza kutembea juu ya maji. Lakini wakati alifika karibu na Yesu, akaangalia zoruba na akaogopa. Akaanza kuzama. Akalalamika: ‘Bwana, uniokoe!’ Yesu akamukamata ku mukono, na kumuuliza: ‘Juu ya nini unakuwa na mashaka? Imani yako iko wapi?’

Yesu na Petro wakapanda mu mashua, na palepale zoruba ikatulia. Unawaza mitume walijisikia namna gani? Walisema: “Uko kabisa Mwana wa Mungu.”

Ile haikukuwa mara ya kwanza yenye Yesu alituliza nguvu za asili. Wakati fulani, Yesu na mitume wake walikuwa mu mashua na walikuwa wanaenda ngambo ingine ya bahari. Wakati walikuwa wanavuka bahari, Yesu alilala usingizi kwenye sehemu ya nyuma ya mashua. Wakati alikuwa analala, kulitokea zoruba kubwa. Mawimbi ilipiga mashua, na maji ilianza kujaa mu mashua. Mitume walimuamusha Yesu. Walilalamika: ‘Mwalimu, tuko karibu kufa! Utusaidie!’ Yesu aliamuka na akaambia bahari: “Nyamaza!” Mara moja, upepo ukatulia na bahari ikakuwa kimya. Kisha Yesu akauliza mitume wake: ‘Imani yenu iko wapi?’ Wakaanza kuambiana: “Hata upepo na bahari vinamutii.” Mitume walijifunza kama, wakimutegemea Yesu kabisa, hakuna kitu kitawaogopesha.

“Ningekuwa wapi kama singekuwa na imani kwamba nitaona wema wa Yehova katika inchi ya wazima?”​—Zaburi 27:13