Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

86

Yesu Anamufufua Lazaro

Yesu Anamufufua Lazaro

Yesu alikuwa na marafiki watatu: Lazaro na dada zake wawili, Maria na Marta. Walikuwa wanaishi Betania. Siku moja, wakati Yesu alikuwa ngambo ingine ya Yordani, Maria na Marta walimutumia ujumbe huu: ‘Lazaro ni mugonjwa sana. Tafazali, ukuje mbio!’ Lakini, Yesu hakuenda palepale. Alingoja kwa siku mbili. Kisha, aliambia wanafunzi wake: ‘Tuende Betania. Lazaro amelala, ninaenda kumuamusha.’ Mitume wakamuambia: ‘Kama Lazaro amelala, ile itamusaidia ajisikie muzuri.’ Kwa hiyo, Yesu akawaambia waziwazi: ‘Lazaro amekufa.’

Wakati Yesu alifika Betania, Lazaro alikuwa amefanya siku ine mu kaburi. Watu mingi sana walikuja kufariji Marta na Maria. Wakati Marta alisikia kama Yesu amefika, alienda haraka ili kumupokea. Alimuambia: “Bwana, kama ungekuwa hapa ndugu yangu hangekufa.” Yesu akamuambia: ‘Ndugu yako atafufuka. Marta, unaamini vile?’ Akajibu: ‘Ninaamini kama atafufuka ku ufufuo wa siku ya mwisho.’ Yesu akamuambia: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.”

Kisha, Marta akaenda kwa Maria na kumuambia: ‘Yesu amefika.’ Maria akaenda haraka kumupokea Yesu, na watu mingi wakamufuata. Wakati alifika karibu na Yesu, akaanguka mbele yake na kuanza kulia sana. Akamuambia Yesu: ‘Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.’ Wakati Yesu aliona namna Maria iko na huzuni sana, yeye pia akaanza kulia. Wakati watu waliona Yesu anatokwa na machozi, wakasema: ‘Yesu alikuwa anamupenda Lazaro sana.’ Lakini wengine wakaanza kuuliza: ‘Juu ya nini hakuzuia rafiki yake asikufe?’ Yesu angefanya nini?

Yesu alienda ku kaburi. Kwa sababu walikuwa wametia jiwe kubwa ku muingilio wa kaburi, Yesu alisema: ‘Mutoshe ile jiwe.’ Marta akamuambia: ‘Lakini kumepita siku ine! Kwa sasa, mwili wake umeanza kunuka.’ Lakini, wakatosha jiwe, na Yesu akasali: ‘Baba, ninakushukuru kwa sababu umenisikia. Ninajua kama unanisikiaka; lakini ninasema kwa sauti ili hawa watu waamini kama ni wewe njo ulinituma.’ Kisha, akaita kwa sauti: “Lazaro, kuja huku inje!” Kisha kukatokea jambo moja la kushangaza: Lazaro akatoka mu kaburi! Kwa sababu alikuwa amefungwa vitambaa, Yesu akasema: ‘Mumufungue, mumuache aende.’

Watu mingi wenye waliona lile jambo wakaanza kumuamini Yesu. Lakini wengine wakaenda na kuambia Wafarisayo. Tangu ile siku, Wafarisayo wakatafuta namna ya kuua Lazaro na Yesu. Yuda Iskariote, mumoja wa wale mitume 12, akaenda kuona Wafarisayo kwa uficho na kuwauliza: ‘Mutanipatia nini kama ninawasaidia kumupata Yesu?’ Wakakubaliana kumupatia vichele 30 vya feza. Kwa hiyo, Yuda akaanza kutafuta nafasi ya kumutoa Yesu kwa Wafarisayo.

“Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu mwenye kuokoa; na Yehova Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi anaokoa katika kifo.”​—Zaburi 68:20