Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

87

Pasaka ya Mwisho ya Yesu

Pasaka ya Mwisho ya Yesu

Kila mwaka, tarehe 14 ya mwezi wa Nisani, Wayahudi walikuwa wanafanya Pasaka. Pasaka ilikuwa inawakumbusha namna Yehova aliwatoshaka katika utumwa wa Misri na kuwaleta katika Inchi ya Ahadi. Mu mwaka wa 33, Yesu na mitume wake walifanyia Pasaka Yerusalemu, mu chumba kimoja cha juu. Wakati walimaliza kula, Yesu alisema: “Mumoja wenu atanisaliti.” Mitume walishituka na kumuuliza: ‘Ni nani?’ Yesu aliwajibu: ‘Ni ule mwenye nitapatia mukate.’ Kisha, akamupatia Yuda Iskariote mukate. Palepale Yuda akasimama na kuenda.

Kisha, Yesu akasali, akagawanya mukate vipande-vipande, na kupatia mitume wenye walikuwa pale. Akawaambia: ‘Mukule mukate huu. Unafananisha mwili wangu, wenye nitatoa kwa ajili yenu.’ Kisha, akasali kwa ajili ya divai, akaichukua na kupatia mitume wake. Akawaambia: ‘Mukunywe hii divai. Inafananisha damu yangu, yenye nitatoa ili zambi zisamehewe. Ninawatolea ahadi kwamba mutakuwa wafalme pamoja na mimi mbinguni. Mukuwe munafanya hivi kila mwaka ili kunikumbuka.’ Njo maana wanafunzi wa Yesu wanakusanyikaka mangaribi ya Nisani 14 kila mwaka. Ule mukutano njo unaitwa Chakula cha Mangaribi cha Bwana.

Kisha kula ile chakula, mitume walianza kubishana juu ya kujua ni nani njo alikuwa mukubwa kati yao. Lakini Yesu aliwaambia: ‘Ule mwenye anajiona kuwa mudogo zaidi kati yenu, njo mukubwa zaidi.’

Kisha akaongeza: ‘Ninyi muko marafiki wangu. Ninawaambia kila kitu chenye Baba yangu anapenda niwaambie. Sasa hivi nitaenda kwa Baba yangu mwenye iko mbinguni, lakini ninyi mutabakia. Watu watajua kama muko wanafunzi wangu wakati wataona namna munapendana. Munapaswa kupendana sawa vile niliwapenda.’

Ku mwisho, Yesu alimuomba Yehova awalinde wanafunzi wake wote. Alimuomba Yehova asaidie wanafunzi wake wafanye kazi kwa amani. Alisali jina la Yehova litakaswe. Kisha, Yesu na mitume wake waliimba nyimbo za kumusifu Yehova na kisha wakaenda inje. Wakati wa kumukamata Yesu ulikuwa umekaribia.

“Musiogope, kundi ndogo, kwa maana Baba yenu amekubali kuwapatia ninyi Ufalme.”​—Luka 12:32