Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

88

Yesu Anakamatwa

Yesu Anakamatwa

Yesu na mitume wake walipita mu Bonde la Kidroni wakati walikuwa wanaenda ku Mulima wa Mizeituni. Ilikuwa usiku na mwezi ulionekana muzima. Wakati walifika mu bustani ya Getsemane, Yesu aliwaambia: “Mubakie hapa na muendelee kukesha.” Kisha, akaenda mbali kidogo mu bustani na akapiga magoti. Alikuwa na wasiwasi sana na alisali. Alimuambia Yehova: “Mapenzi yako yatendeke.” Kisha, Yehova alituma malaika amutie Yesu moyo. Wakati Yesu alirudia kwenye mitume walikuwa, alikuta wamelala. Akawaambia: ‘Muamuke! Hii haiko wakati wa kulala! Sasa hivi nitatiwa mu mikono ya maadui wangu.’

Kisha wakati kidogo, Yuda akafika. Alikuwa na watu mingi wenye walikuwa na mipanga na fimbo. Alijua kwenye Yesu alikuwa kwa sababu alizoea kuenda na Yesu mu ile bustani. Yuda aliambia maaskari kama atawaonyesha Yesu. Kwa hiyo, alienda kwenye Yesu alikuwa na kusema: ‘Jambo, Mwalimu,’ na kisha, akamubusu. Yesu akamuuliza: ‘Yuda, unanisaliti kwa kunibusu?’

Yesu akaenda karibu na wale watu na kuwauliza: “Munatafuta nani?” Wakasema: “Yesu Munazareti.” Akawajibu: “Ni mimi.” Mara moja wale watu wakarudia nyuma na kuanguka chini. Yesu akawauliza tena: “Munatafuta nani?” Tena wakamujibu: “Yesu Munazareti.” Yesu akawajibu: ‘Nimewaambia kama ni mimi. Muache hawa waende.’

Wakati Petro aliona vile, akakamata upanga wake na kukata sikio la Malko, mutumishi wa kuhani mukubwa. Lakini Yesu aligusa sikio la Malko na kumuponyesha. Kisha, akamuambia Petro: ‘Rudisha upanga wako kwenye uliutosha. Ukipigana kwa upanga, utakufa kwa upanga.’ Kisha maaskari wakamukamata Yesu na kumufunga mikono, lakini mitume wakakimbia. Kisha wakamupeleka Yesu kwa Anasi, kuhani mukubwa. Anasi akamuuliza Yesu maulizo mingi, kisha akamutuma kwa Kayafa, mwenye alikuwa kuhani mukubwa ile mwaka. Lakini nini njo ilifikia mitume?

“Katika ulimwengu mutapata taabu, lakini musiogope! Mimi nimeshinda ulimwengu.”​—Yohana 16:33