Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

90

Yesu Anakufa Kule Golgota

Yesu Anakufa Kule Golgota

Wakubwa wa makuhani walimukamata Yesu na kumupeleka ku nyumba ya gavana. Pilato akawauliza: ‘Munasema huyu mutu alifanya kosa gani?’ Wakajibu: ‘Anasema iko mufalme!’ Pilato akamuuliza Yesu, ‘Wewe ni Mufalme wa Wayahudi?’ Yesu akajibu: ‘Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu.’

Kisha, Pilato akamutuma Yesu kwa Herode, mutawala wa Galilaya. Alipenda aone kama Herode naye atamupata Yesu na kosa fulani. Lakini Herode hakumupata Yesu na kosa lolote na akamurudisha kwa Pilato. Kisha, Pilato akaambia watu: ‘Mimi na Herode tumeona kama huyu mutu hana kosa. Nitamuachilia.’ Watu wengi wakalalamika: ‘Umuue! Umuue!’ Maaskari wakamupiga Yesu fimbo, wakamutemea mate, na kumupiga. Wakamuvalisha taji ya miiba ku kichwa na walikuwa wanamuchekelea na kusema, ‘Jambo, Mufalme wa Wayahudi.’ Pilato akaambia tena watu: ‘Huyu mutu hana kosa.’ Lakini wakalalamika: ‘Atundikwe ku muti!’ Basi, Pilato akawapatia Yesu ili waende kumuua.

Maaskari wakamupeleka Yesu fasi yenye iliitwa Golgota. Wakamupigilia misumari ku muti na kisha wakasimamisha ile muti. Yesu akasali: ‘Baba, uwasamehe kwa sababu hawajue jambo lenye wanafanya.’ Watu wakamuchekelea Yesu. Walikuwa wanasema: ‘Kama uko Mwana wa Mungu, shuka ku muti! Ujiokoe.’

Mutenda-mabaya mumoja mwenye alikuwa ametundikwa pembeni yake akasema: ‘Unikumbuke wakati utaingia mu Ufalme wako.’ Yesu akamuambia: ‘Utakuwa pamoja na mimi mu Paradiso.’ Wakati ilikuwa saa sita, inchi yote ikakuwa na giza, na ile giza ikafanya saa tatu. Wanafunzi fulani wakasimama pembeni ya ile muti. Kati yao kulikuwa Maria, mama ya Yesu. Yesu akaomba Yohana amuchunge Maria sawa vile mama yake muzazi.

Ku mwisho, Yesu akasema: “Imetimizwa!” Akainamisha kichwa na akakufa. Palepale, tetemeko kubwa la inchi likatokea. Pazia (rideau) lenye lilikuwa kati ya Patakatifu na Patakatifu Zaidi, likapasuka katikati. Mukubwa mumoja wa maaskari akasema: ‘Huyu alikuwa kabisa Mwana wa Mungu.’

“Hata ahadi za Mungu zikuwe nyingi namna gani, zimekuwa ‘ndiyo’ kupitia yeye.”​—2 Wakorinto 1:20