Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

91

Yesu Anafufuliwa

Yesu Anafufuliwa

Kisha Yesu kufa, mwanaume fulani tajiri, mwenye aliitwa Yosefu, alimuomba Pilato ruhusa ya kutosha mwili wa Yesu ku muti. Yosefu alifunga mwili wa Yesu kwa nguo ya muzuri na kuupakaa manukato, na akautia mu kaburi la mupya. Kisha aliviringisha jiwe kubwa ku muingilio wa lile kaburi. Wakubwa wa makuhani waliambia Pilato: ‘Kama hatufanye kitu, wanafunzi wake watakamata mwili wake na kusema kama amefufuliwa.’ Basi Pilato akawaambia: ‘Mufunge muingilio wa kaburi na mutie pale watu wa kuchunga ile kaburi.’

Kisha siku tatu, asubui sana, wanamuke fulani walienda ku kaburi na wakaona kama hakuna tena jiwe ku muingilio wa kaburi. Malaika alikuwa ndani ya kaburi, na aliambia wale wanamuke hivi: ‘Musiogope. Yesu amefufuliwa. Muambie wanafunzi wake waende kukutana naye kule Galilaya.’

Wakati Maria Magdalene alikutana na Petro na Yohana, aliwaambia: ‘Kuko mutu mwenye ameiba mwili wa Yesu!’ Petro na Yohana wakaenda mbio ku kaburi. Wakati walikuta kaburi liko wazi, wakarudia kwao.

Wakati Maria alirudia ku kaburi, aliona malaika wawili ndani ya kaburi. Akawaambia: ‘Sijue kwenye walimupeleka Bwana wangu.’ Kisha akaona mwanaume fulani, akawaza ni mutu wa kuchunga bustani. Akamuambia: ‘Tafazali, uniambie kwenye ulimutia.’ Ule mwanaume akasema: “Maria!” Mara moja Maria akatambua kama ni Yesu. Akalalamika hivi: “Mwalimu!” na akamukumbatia. Yesu akamuambia: ‘Uende uambie ndugu zangu kama umeniona.’ Palepale, Maria akaenda mbio kuona wanafunzi na kuwaambia kama amemuona Yesu.

Kisha, ileile siku, wanafunzi mbili walikuwa wanatoka Yerusalemu na kuenda Emau. Mwanaume fulani akaanza kuenda pamoja nao. Akawauliza: ‘Muko munazungumuzia juu ya jambo gani?’ Wakajibu: ‘Haujasikia mambo yenye ilitokea? Kumepita siku tatu tangu wakubwa wa makuhani wamuue Yesu. Na sasa wanamuke fulani wako wanasema kama iko muzima!’ Ule mwanaume akawauliza: ‘Hamuamini mambo yenye manabii walisemaka? Walisemaka kama Kristo atakufa na kisha atafufuliwa.’ Na akaendelea kuwafasiria Maandiko. Wakati walifika Emau, wanafunzi wakamuomba ule mwanaume asiende. Wakati walikuwa wanakula chakula cha mangaribi, ule mwanaume akasali kwa ajili ya mukate. Mara moja, wale wanafunzi wakatambua kama ni Yesu. Kisha hakuonekana tena pale.

Wale wanafunzi mbili wakaenda mara moja Yerusalemu kwenye mitume walikuwa wamekusanyika, na wakawaambia mambo yenye waliona. Wakati walikuwa wote mu nyumba, Yesu akawatokea. Ku mwanzo, mitume hawakuamini kama ni Yesu. Kwa hiyo akawaambia: ‘Muangalie mikono yangu; muniguse. Maandiko ilisemaka kama Kristo alipaswa kufufuka.’

“Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.”​—Yohana 14:6