Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

93

Yesu Anarudia Mbinguni

Yesu Anarudia Mbinguni

Yesu alikutana na wanafunzi wake kule Galilaya. Aliwapatia amri hii ya maana sana: ‘Muende mufanye wanafunzi mu inchi zote. Muwafundishe mambo yenye niliwafundisha, na muwabatize.’ Kisha aliwatolea ahadi hii: ‘Musisahau: Nitakuwa pamoja na ninyi kila siku.’

Kwa siku 40 kisha Yesu kufufuliwa, alitokea wanafunzi wengi katika Galilaya na Yerusalemu. Aliwafundisha mambo ya maana na alifanya miujiza mingi. Kisha, Yesu alikutana na mitume wake mara ya mwisho, ku Mulima wa Mizeituni. Aliwaambia: ‘Musitoke Yerusalemu. Muendelee kungoja ahadi yenye Baba aliwatolea.’

Lakini mitume hawakuelewa. Basi wakamuuliza: ‘Ni wakati huu njo utakuwa Mufalme wa Israeli?’ Yesu akawajibu: ‘Wakati wa Yehova kuniweka nikuwe Mufalme haujafika. Karibuni, mutapokea roho takatifu. Na itawapatia nguvu. Kisha, mutakuwa mashahidi wangu. Muende muhubiri katika Yerusalemu, Yudea, Samaria, na mupaka sehemu za mbali sana za dunia.’

Kisha Yesu akainuliwa juu katika anga na mawingu ikamufunika. Wanafunzi wake wakaendelea kuangalia juu, lakini hawakumuona tena.

Halafu, wanafunzi wakatoka ku Mulima wa Mizeituni na kuenda Yerusalemu. Walikuwa wanakutana pamoja mu chumba cha juu na walikuwa wanasali. Walikuwa wanangoja Yesu awapatie maagizo ingine.

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”​—Matayo 24:1