Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

94

Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu

Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu

Siku kumi kisha Yesu kurudia mbinguni, wanafunzi wake walipokea roho takatifu. Ilikuwa Sikukuu ya Pentekoste ya mwaka wa 33. Watu wa sehemu mbalimbali walikuwa wamekuja Yerusalemu kwa ajili ya ile Sikukuu. Wanafunzi wa Yesu 120 hivi walikuwa wamekusanyika mu chumba cha juu cha nyumba fulani. Mara moja, jambo la kushangaza likatokea. Kitu fulani kama moto kikaonekana juu ya kichwa cha kila mwanafunzi, na wakaanza kusema luga mbalimbali. Makelele sawa vile makelele ya upepo wenye nguvu ikajaa mu ile nyumba.

Wageni wenye walitoka sehemu mbalimbali na kuja Yerusalemu walisikia ile makelele na kuenda mbio ku ile nyumba ili waone kama kulitokea nini. Walishangaa wakati walisikia wanafunzi wanazungumuza zile luga mbalimbali. Wakasema: ‘Hawa watu ni Wagalilaya, mbona wako wanasema luga zetu?’

Kisha Petro na mitume wengine wakasimama mbele ya watu mingi. Petro akawaelezea namna Yesu aliuawa na kama Yehova alimufufua. Petro akasema: ‘Sasa Yesu iko mbinguni ku mukono wa kuume wa Mungu, naye ametupatia roho takatifu kama vile alituambiaka. Njo maana mumeona na kusikia hii miujiza.’

Maneno yenye Petro alisema iligusa watu moyo. Kwa hiyo, wakauliza: “Inaomba tufanye nini?” Petro akawaambia: ‘Mutubu zambi zenu na mubatizwe katika jina la Yesu. Na ninyi pia, mutapokea zawadi ya roho takatifu.’ Ile siku, watu karibu 3000 wakabatizwa. Kuanzia ile wakati, hesabu ya wanafunzi ikaongezeka haraka katika Yerusalemu. Kwa musaada wa roho takatifu, mitume wakaanzisha makutaniko mingi ili waweze kufundisha wanafunzi mambo yote yenye Yesu alikuwa amewaagiza.

“Kama unatangaza mbele ya watu wote kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana, na unaonyesha imani katika moyo wako kwamba Mungu alimufufua kutoka kwa wafu, utaokolewa.”​—Waroma 10:9