Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

97

Kornelio Anapokea Roho Takatifu

Kornelio Anapokea Roho Takatifu

Mu muji wa Kaisaria, mulikuwa mukubwa mumoja wa maaskari mwenye aliitwa Kornelio. Hakukuwa Muyahudi, lakini Wayahudi walikuwa wanamuheshimia sana. Alikuwa anasaidia maskini. Alimuamini Yehova na alikuwa anasali kwa ukawaida. Siku moja, malaika alimutokea Kornelio na kumuambia: ‘Mungu amesikia sala zako. Sasa utume wanaume mu muji wa Yopa, kwenye Petro iko, na umuombe akuje kwako.’ Palepale, Kornelio akatuma wanaume tatu Yopa. Ule muji ulikuwa ku kilometre 50 hivi upande wa kusini wa Kaisaria.

Ile wakati, mu muji wa Yopa, Petro alipata maono. Aliona wanyama wenye Wayahudi hawakuruhusiwa kula, na alisikia sauti inamuambia akule wale wanyama. Petro akasema: ‘Sijakulaka munyama mwenye haiko safi.’ Ile sauti ikamuambia: ‘Usiseme kama wale wanyama hawako safi. Mungu alishawafanya wakuwe safi.’ Ile sauti ikasema tena: ‘Wanaume tatu wako mbele ya mulango wako. Uende nao.’ Petro akaenda ku mulango na kuwauliza wale wanaume kama walikuwa wanatafuta nini. Wakajibu: ‘Kornelio, mukubwa wa maaskari wa Roma, njo mwenye alitutuma. Inaomba uende kwake, kule Kaisaria.’ Petro akawaomba wabakie kwake ule usiku. Siku yenye ilifuata, akaenda nao mu muji wa Kaisaria, pamoja na ndugu fulani wa Yopa.

Wakati Kornelio aliona Petro, akapiga magoti mbele yake. Lakini Petro akamuambia: ‘Simama! Niko tu mutu kama wewe. Kwa kawaida, Wayahudi hawaingiake mu nyumba za Watu wa Mataifa, lakini Mungu aliniambia nikuje kwako. Sasa, tafazali uniambie juu ya nini ulituma watu waniite.’

Kornelio akamuambia Petro: ‘Kumepita siku ine, nilikuwa ninamuomba Mungu, na malaika fulani aliniambia nitume watu wakuite. Tafazali, utufundishe maneno ya Yehova.’ Petro akasema: ‘Nimeelewa kama Mungu hana ubaguzi. Anakubali kila mutu mwenye anapenda kumuabudu.’ Petro akawafundisha mambo mingi juu ya Yesu. Kisha roho takatifu ikashuka juu ya Kornelio na juu ya wote wenye walikuwa pamoja naye, na wote wakabatizwa.

“Katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa [Mungu] na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.” ​—Matendo 10:35