Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

99

Mulinzi wa Gereza Anajifunza Kweli

Mulinzi wa Gereza Anajifunza Kweli

Kule Filipi, kulikuwa mutumishi mumoja mwanamuke mwenye alikuwa na pepo muchafu. Ule pepo alitumikisha ule kijana mwanamuke juu ya kutabiri mambo yenye itatokea, na ile ilikuwa inaletea mabwana wake faida mingi. Wakati Paulo na Sila walifika Filipi, ule kijana mwanamuke aliendelea kuwafuata kwa siku mingi. Ule pepo muchafu alifanya ule kijana mwanamuke alalamike: “Watu hawa ni watumwa wa Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi.” Ku mwisho, Paulo aliambia ule pepo muchafu: ‘Katika jina la Yesu, ninakuagiza utoke ndani yake!’ Mara moja ule pepo muchafu akatoka.

Wakati mabwana wake waliona kama hawawezi tena kupata feza kupitia ule kijana mwanamuke, walikasirika sana. Walikokota Paulo na Sila mupaka kwa waamuzi wa raia na kusema: ‘Watu hawa wanavunja sheria na wanasumbua sana muji wote!’ Wale waamuzi wakaamuru Paulo na Sila wapigwe na kutupwa mu gereza. Mulinzi wa gereza akawatupa mu chumba cha ndani sana cha gereza, mwenye mulikuwa giza sana, na kufunga miguu yao mu mikatale.

Paulo na Sila walimusifu Yehova kwa wimbo, na wafungwa wengine walikuwa wanawasikiliza. Mara moja, katikati ya usiku, tetemeko kubwa la inchi likatokea na kutikisa misingi ya gereza. Milango ya gereza ilifunguka na minyororo na mikatale yenye walikuwa wamefungwa ikafunguka. Mulinzi wa gereza akaingia mbio ndani ya gereza na akaona kama milango ya gereza ilikuwa imefunguka. Kwa sababu aliwaza kama wafungwa wote walishakimbia, akakamata upanga ili ajiue.

Lakini Paulo akasema hivi kwa sauti: ‘Usijiue! Sisi wote tuko hapa!’ Ule mulinzi akaingia na kuanguka chini mbele ya Paulo na Sila. Akawauliza: “Nifanye nini ili niokolewe?” Wakamuambia: ‘Wewe na watu wa nyumba yako munapaswa kumuamini Yesu.’ Basi, Paulo na Sila wakawafundisha neno la Yehova, na ule mulinzi wa gereza na watu wa nyumba yake wakabatizwa.

“Watu watawakamata ninyi na kuwatesa na kuwatoa kwenye masinagogi na kuwatia katika magereza. Mutapelekwa mbele ya wafalme na magavana kwa ajili ya jina langu. Hilo litawapatia ninyi nafasi ya kutoa ushahidi.”​—Luka 21:12, 13