Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

101

Paulo Anapelekwa Roma

Paulo Anapelekwa Roma

Safari ya tatu ya Paulo ya umisionere iliishia Yerusalemu. Kule, walimukamata na kumutupa mu gereza. Usiku, Yesu alimuambia katika maono: ‘Utaenda Roma na kuhubiri kule.’ Walimutosha Paulo Yerusalemu na kumupeleka Kaisaria, na kule alifanya miaka mbili mu gereza. Wakati alikuwa anasamba mbele ya Gavana Festo, Paulo alisema: ‘Nitahukumiwa na Kaisari, kule Roma.’ Festo akamuambia: ‘Vile unapenda uende kusamba mbele ya Kaisari; utaenda kwa Kaisari.’ Kwa hiyo, walimupandisha Paulo mu mashua ya kuenda Roma. Ndugu wawili Wakristo, Luka na Aristarko, walienda pamoja naye.

Zoruba kali ilitokea mu bahari, na ilifanya siku mingi. Watu wenye walikuwa mu ile mashua waliwaza kama watakufa. Lakini Paulo aliwaambia: ‘Wanaume, malaika wameniambia katika ndoto: “Usiogope, Paulo. Utafika Roma, na wale wote wenye wanasafiri pamoja na wewe watafika salama.” Kwa hiyo, musiogope! Hatutakufa.’

Zoruba iliendelea kwa siku 14. Ku mwisho, waliona inchi kavu kwa mbali. Ilikuwa kisiwa (île) cha Malta. Mashua yao iligonga mwamba na kuvunjika vipande-vipande, lakini watu wote 276 wenye walikuwa ndani ya mashua, walifika salama kwenye inchi kavu. Wamoja waliogelea na wengine walikamata ku vipande vya mashua na kuenda mupaka pembeni ya bahari. Watu wa Malta waliwasaidia na hata waliwasha moto ili waote na kupata kifukutu.

Kisha miezi tatu, maaskari walimupeleka Paulo Roma kwa kutumia mashua ingine. Wakati alifika, ndugu walikuja kumupokea. Wakati aliwaona, Paulo alimushukuru Yehova na alipata nguvu. Hata kama Paulo alikuwa mufungwa, aliruhusiwa kuishi mu nyumba ya kulipia, na askari alikuwa anamuchunga. Aliishi pale miaka mbili. Watu walikuwa wanakuja kumuona, na alikuwa anawahubiria juu ya Yesu na juu ya Ufalme wa Mungu. Tena, Paulo aliandikia barua makutaniko ya Asia Ndogo na Yudea. Kwa kweli, Yehova alimutumikisha Paulo ili kuhubiri habari njema kwa mataifa.

“Katika kila njia tunajipendekeza sisi wenyewe kuwa watumishi wa Mungu, kwa kuvumilia mambo mengi, kwa taabu, kwa nyakati za uhitaji, kwa magumu.”​—2 Wakorinto 6:4