Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 103

“Ufalme Wako na Uje”

“Ufalme Wako na Uje”

Yehova anaahidi hivi: ‘Hakutakuwa tena na kilio, maumivu, magonjwa, au kifo. Nitafuta kila chozi kutoka katika macho yao. Mambo yote mabaya ya zamani yatasahauliwa.’

Yehova aliwaweka Adamu na Hawa katika bustani ya Edeni ili waishi kwa furaha na amani. Walipaswa kumwabudu Baba yao wa mbinguni na kuijaza dunia. Adamu na Hawa hawakumtii Yehova, lakini kusudi lake halikubadilika. Katika kitabu hiki tumeona kwamba kila kitu ambacho Mungu ameahidi lazima kitimie. Ufalme wake utaleta baraka nzuri ajabu duniani, kama alivyomwahidi Abrahamu.

Hivi karibuni, Shetani, roho wake waovu, na watu wote wabaya hawatakuwepo. Kila mtu aliye hai atamwabudu Yehova. Hatutakuwa wagonjwa wala hatutakufa. Badala yake, kila siku tutaamka tukiwa wenye nguvu na wenye furaha kwa sababu tuko hai. Dunia itakuwa paradiso. Kila mtu atakuwa na chakula kizuri na kuishi kwa usalama. Watu watakuwa wenye fadhili, si wakatili au wenye jeuri. Hatutahofu wanyama-mwitu, nao pia hawatatuogopa.

Itakuwa pindi yenye kusisimua sana wakati ambapo Yehova ataanza kuwafufua watu. Tutawakaribisha wale walioishi nyakati za kale kama vile Abeli, Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Ruthu, Esta, na Daudi. Watashirikiana nasi kuifanya Dunia iwe paradiso. Siku zote kutakuwa na kazi nyingi zenye kufurahisha.

Yehova anataka uishi katika paradiso. Utapata nafasi ya kujifunza mambo mengi zaidi kumhusu. Acheni kila siku tuendelee kumkaribia Yehova zaidi na zaidi, sasa na milele!

“Unastahili, Ee Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.”​—Ufunuo 4:11