Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

103

‘Ufalme Wako Ukuje’

‘Ufalme Wako Ukuje’

Yehova alitoa ahadi hii: ‘Hakutakuwa tena kilio, maumivu, magonjwa, wala kifo. Nitapanguza machozi yote kutoka katika macho yao. Mambo yote ya mubaya ya zamani itasahauliwa.’

Yehova alitia Adamu na Eva mu bustani ya Edeni. Alipenda waishi kwa furaha na amani. Walipaswa kumuabudu Baba yao wa mbinguni na kujaza dunia. Adamu na Eva hawamukutii Yehova, lakini kusudi la Yehova halikubadilika. katika hiki kitabu, tumeona kama mambo yote yenye Mungu anasemaka haikosake kutimia. Ufalme wake utaleta baraka za muzuri sana mu dunia, sawa vile alimuambiaka Abrahamu.

Karibuni, Shetani na pepo wake wachafu wataharibiwa, na watu wote wabaya hawatakuwa tena ku dunia. Kila mutu atamuabudu Yehova. Magonjwa itaisha, na kifo kitaisha. Kila siku, tutaamuka na nguvu na furaha. Dunia itakuwa paradiso. Kila mutu atakuwa na chakula kizuri na ataishi mu nyumba yake bila kuogopa. Watu watakuwa wapole. Watatendeana muzuri. Hatutaogopa wanyama wa pori, nao hawatatuogopa.

Itakuwa muzuri sana wakati Yehova ataanza kufufua watu! Tutafurahi kuonana na Abeli, Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Rutu, Esta, Daudi na wengine wenye walimutumikiaka Mungu zamani. Tutatumika nao ili kufanya dunia ikuwe paradiso. Sikuzote tutakuwa na kazi mingi ya kufurahisha.

Yehova anapenda ukuwe katika paradiso. Katika paradiso, utafikia kumujua mu namna yenye hauwezi hata kuwazia sasa. Tuendelee basi kumukaribia Yehova zaidi na zaidi, kuanzia sasa mupaka milele!

“Unastahili, Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.”​—Ufunuo 4:11