Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Barua ya Baraza Lenye Kuongoza

Barua ya Baraza Lenye Kuongoza

Ndugu na Dada Zetu Wapendwa:

Sisi waabudu wa Yehova, tunapenda Neno lake, Biblia. Tuko hakika kama iko na historia yenye haina makosa, inatutolea mashauri ya muzuri sana mu kila sehemu ya maisha yetu, na iko na habari zenye kugusa moyo zenye kuonyesha kama Yehova anapenda wanadamu. (Zaburi 119:105; Luka 1:3; 1 Yohana 4:19) Tunapenda sana kusaidia wengine wajifunze kweli za maana sana zenye kuwa ndani ya Neno la Mungu. Kwa hiyo, tunafurahi sana kuwatolea kitabu, “Mambo Yenye Unaweza Kujifunza Katika Biblia.” Tunapenda kuwaelezea mambo fulani juu ya hiki kitabu.

Hiki kitabu kimetayarishwa zaidi sana kwa ajili ya watoto. Lakini, tunaweza kukitumia tena ili kusaidia hata watu wakubwa wenye wanapenda kujifunza mambo mingi zaidi juu ya Biblia. Na kwa sababu Biblia ni kitabu cha watu wote, sisi wote tutapata faida kwa kuchunguza mambo yenye kuwa ndani, yenye inaweza kutusaidia tukuwe na furaha ya kweli.

Hiki kitabu kinatumia habari zenye kuwa ndani ya Biblia ili kueleza historia ya familia ya wanadamu kuanzia wakati wa uumbaji na kuendelea. Tumejikaza sana ili kueleza habari zenye kuwa ndani ya Biblia kwa njia mwepesi na yenye kuwa wazi. Tena, tumejikaza sana ili kuzieleza namna zilifuatana.

Lakini, hiki kitabu hakieleze tu habari zenye kuwa ndani ya Biblia. Maandishi na picha vimetayarishwa kwa njia yenye kufanya hizi habari zionekane kuwa za kweli kabisa na zionyeshe namna watu wenye kuzungumuziwa walijisikia.

Hiki kitabu kinatusaidia kuona kama Biblia ni kitabu chenye kuzungumuzia wanaume na wanamuke wenye walimutii Yehova na wale wenye hawakumutii. Na kinatusaidia tujifunze kupitia mifano yao. (Waroma 15:4; 1 Wakorinto 10:6) Hiki kitabu kiko na sehemu 14. Ku mwanzo wa kila sehemu kuko maelezo ya mufupi juu ya mambo yenye tunaweza kujifunza.

Kama uko muzazi, unaweza kusoma hadisi moja pamoja na mutoto wako kisha munaweza kuzungumuzia picha yenye kupatana na ile hadisi. Kisha munaweza kusoma maandiko ya Biblia yenye kuzungumuzia hadisi yenye munajifunza. Umusaidie mutoto wako apatanishe mambo yenye anasoma mu Biblia na hadisi yenye munajifunza mu hiki kitabu. Tunaweza kutumia tena hii njia wakati tunasaidia mutu mukubwa aelewe kwa kifupi ujumbe wenye kuwa mu Biblia.

Tunatumaini kama hiki kitabu kitasaidia watu wote wenye kuwa na moyo muzuri, ikuwe vijana ao wazee, wajifunze mambo ya maana yenye kuwa ndani ya Neno la Mungu na waitumikishe mu maisha yao. Kisha, wanaweza kumuabudu Yehova pamoja na familia yake yenye anapenda sana.

Ndugu zenu,

Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova