Utangulizi wa Sehemu ya 1
Biblia inaanza na habari ya uumbaji. Inatusaidia tuone vitu mingi vya muzuri vyenye Yehova ameumba, ikuwe mbinguni ao ku dunia. Kama uko muzazi, umusaidie mutoto wako aone vitu mbalimbali vya kushangaza vyenye Yehova aliumba. Umuelezee kama Mungu aliumba wanadamu ili wakuwe wa hali ya juu sana kupita wanyama. Alitupatia uwezo wa kuzungumuza, kufikiri, kufanya vitu, kuimba, na kusali. Umusaidie afurahie uwezo na hekima ya Yehova na zaidi sana upendo wake kwa kila mumoja wetu, na kwa viumbe wote.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 1
Mungu Aliumba Mbingu na Dunia
Biblia inasema kama Mungu aliumba mbingu na dunia. Juu ya nini aliumba kwanza malaika mumoja mbele ya kuumba kila mutu na kila kitu?
SOMO LA 2
Mungu Aliumba Mwanaume na Mwanamuke wa Kwanza
Mungu aliumba mwanaume na mwanamuke wa kwanza na akawatia mu bustani ya Edeni. Alitaka waanzishe familia na wafanye dunia yote ikuwe paradiso.