Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi wa Sehemu ya 3

Utangulizi wa Sehemu ya 3

Baada ya Gharika, Biblia inasimulia kuhusu watu wachache waliomtumikia Yehova. Mmoja wao ni Abrahamu, aliyejulikana kuwa rafiki ya Yehova. Kwa nini aliitwa rafiki ya Yehova? Ikiwa wewe ni mzazi, mfundishe mtoto wako kwamba Yehova anampenda kibinafsi na anataka kumsaidia. Kama Abrahamu na wanaume wengine waaminifu, kama vile Loti na Yakobo, tunaweza kumwomba Yehova atusaidie. Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atatimiza ahadi zake zote.

KATIKA SEHEMU HII

Mnara wa Babeli

Baadhi ya watu waliamua kujenga jiji na mnara ambao kilele chake kingefika mbinguni. Kwa nini Mungu alifanya wazungumze lugha tofauti-tofauti?

Abrahamu na Sara Walimtii Mungu

Kwa nini Abrahamu na Sara waliacha maisha yao mazuri na kuhamia nchi ya Kanaani?

Hatimaye Wapata Mtoto!

Mungu alitimizaje ahadi yake kwa Abrahamu? Ni mtoto yupi wa Abrahamu aliyehusika, Isaka au Ishmaeli?

Mkumbuke Mke wa Loti

Mungu alinyesha mvua ya moto na kiberiti katika majiji ya Sodoma na Gomora. Kwa nini majiji hayo yaliharibiwa? Kwa nini tunapaswa kumkumbuka mke wa Loti?

Jaribu la Imani

Mungu alimwambia Abrahamu hivi: ‘Tafadhali, mchukue mwana wako wa pekee na umtoe akiwa dhabihu kwenye mmoja kati ya milima ya Moria.’ Abrahamu alikabili jinsi gani jaribu hilo la imani?

Yakobo Alipewa Urithi

Isaka na Rebeka walikuwa na watoto wawili mapacha, Esau na Yakobo. Kwa kuwa Esau alikuwa mzaliwa wa kwanza, angepata urithi wa pekee. Kwa nini aliuza haki hiyo kwa bakuli la mchuzi?

Yakobo na Esau Wafanya Amani

Yakobo alipata jinsi gani baraka kutoka kwa malaika? Na alifanyaje amani na Esau?