Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi wa Sehemu ya 4

Utangulizi wa Sehemu ya 4

Katika sehemu hii tutajifunza kuhusu Yosefu, Ayubu, Musa, na Waisraeli. Wote walivumilia mambo mengi mabaya kutoka kwa Ibilisi. Baadhi yao walitendewa isivyo haki, wakafungwa gerezani, wakawa watumwa, na hata wengine wakauawa. Hata hivyo, Yehova aliwalinda katika njia mbalimbali. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako aelewe jinsi ambavyo watumishi hao wa Yehova walivumilia mambo mabaya bila kuruhusu imani yao idhoofike.

Yehova alileta Mapigo Kumi ili kuonyesha yeye ni mwenye nguvu kuliko miungu yote ya Wamisri. Kazia jinsi ambavyo Yehova aliwalinda watu wake wakati uliopita na jinsi anavyofanya hivyo leo.

KATIKA SEHEMU HII

Mtumwa Aliyemtii Mungu

Yosefu alifanya mambo mazuri, lakini bado aliteseka sana. Kwa nini?

Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe

Ingawa Yosefu alikuwa mbali na familia yao, Mungu alimthibitishia kwamba alikuwa pamoja naye.

Ayubu Alikuwa Nani?

Alimtii Yehova hata ilipokuwa vigumu.

Musa Aliamua Kumwabudu Yehova

Alipokuwa mtoto, Musa aliokolewa kwa sababu ya hekima ya mama yake.

Mti Unaowaka Moto

Kwa nini moto haukuuteketeza mti huo?

Mapigo Matatu ya Kwanza

Farao aliwasababishia watu wake msiba kwa sababu kiburi kilimzuia achukue hatua moja tu rahisi.

Mapigo Sita Yaliyofuata

Mapigo hayo yalitofautianaje na mapigo matatu ya kwanza?

Pigo la Kumi

Pigo la mwisho lilikuwa baya sana hivi kwamba hata Farao mwenye kiburi alikubali mwishowe kuwaruhusu Waisraeli waondoke.

Muujiza Katika Bahari Nyekundu

Farao aliokoka mapigo kumi, lakini je, aliokoka muujiza huu wa Mungu?