Utangulizi wa Sehemu ya 4
Mu hii sehemu tutajifunza juu ya Yosefu, Yobu, Musa, na Waisraeli. Wote walivumilia mambo ya mingi ya mubaya yenye Shetani aliwaletea. Wamoja kati yao walitendewa bila haki, walifungwa mu gereza, walikuwa watumwa, na hata waliuawa. Lakini, Yehova aliwalinda mu njia mbalimbali. Kama uko muzazi, umusaidie mutoto wako aelewe namna wale watumishi wa Yehova walivumilia mambo ya mubaya bila kupoteza imani yao.
Yehova alileta Mapigo Kumi ili kuonyesha kama iko na nguvu kupita miungu yote ya Wamisri. Onyesha namna Yehova alilinda watu wake wakati wenye ulipita na namna anawalinda leo.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 14
Mutumwa Mwenye Alimutii Mungu
Yosefu alifanya mambo ya muzuri, lakini aliteseka sana. Juu ya nini?
SOMO LA 15
Yehova Hakumusahau Yosefu Hata Kidogo
Hata kama Yosefu alikuwa mbali na familia yao, Mungu alimuonyesha kama alikuwa pamoja naye.
SOMO LA 17
Musa Alichagua Kumuabudu Yehova
Wakati alikuwa mutoto, Musa aliokolewa kwa sababu ya hekima ya mama yake.
SOMO LA 19
Mapigo Tatu ya Kwanza
Farao aliletea watu wake matatizo juu kiburi kilifanya akatae kufanya jambo moja tu.
SOMA LA 21
Pigo ya Kumi
Hii pigo ilikuwa mubaya sana na ilifanya Farao mwenye kiburi aache Waisraeli waende.
SOMO LA 22
Muujiza ku Bahari Nyekundu
Farao alipona wakati wa ile mapigo kumi, lakini je, aliokoka muujiza huu wa Mungu?