Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi wa Sehemu ya 5

Utangulizi wa Sehemu ya 5

Miezi miwili baada ya kuvuka Bahari Nyekundu, Waisraeli walifika kwenye Mlima Sinai. Wakiwa hapo, Yehova alifanya agano pamoja na Waisraeli ili wawe taifa lake la pekee. Aliwalinda na kuwaandalia kila kitu walichohitaji—aliwapa mana ili wale, mavazi ya kuvaa, na mahali salama pa kuishi. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako aelewe kwa nini Yehova aliwapa Waisraeli Sheria, maskani, na ukuhani. Kazia umuhimu wa kutimiza mambo tunayoahidi, kuendelea kuwa wanyenyekevu, na sikuzote kudumisha ushikamanifu kwa Yehova.

KATIKA SEHEMU HII

Waisraeli Wamtolea Yehova Ahadi

Waisraeli walimtolea Mungu ahadi ya pekee walipokuwa wamepiga kambi kwenye Mlima Sinai.

Walivunja Ahadi Yao

Musa alipokuwa akipewa zile Amri Kumi, watu walitenda dhambi nzito.

Maskani ya Ibada

Hema hilo la pekee lilikuwa na sanduku la agano.

Wale Wapelelezi Kumi na Wawili

Ripoti ya Yoshua na Kalebu ilikuwa tofauti na ya wale wapelelezi wengine kumi ambao waliipeleleza nchi ya Kanaani.

Walimwasi Yehova

Kora, Dathani, Abiramu, na wanaume wengine 250 walikosa kutambua jambo fulani muhimu kumhusu Yehova.

Punda wa Balaamu Azungumza

Punda aliona mtu ambaye Balaamu hangeweza kumwona.