Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi wa Sehemu ya 6

Utangulizi wa Sehemu ya 6

Waisraeli walipofika Nchi ya Ahadi, maskani ikawa kitovu cha ibada. Makuhani waliwafundisha watu Sheria, na waamuzi wakaongoza taifa hilo. Sehemu hii inaonyesha jinsi maamuzi na matendo ya mtu yanavyoweza kuwaathiri sana watu wengine. Kila Mwisraeli alikuwa na wajibu mbele za Yehova na kwa watu wengine. Onyesha jinsi mifano mizuri ya Debora, Naomi, Yoshua, Hana, binti ya Yeftha, na Samweli ilivyowachochea wengine. Kazia kwamba hata watu fulani ambao hawakuwa Waisraeli, kama vile Rahabu, Ruthu, Yaeli, na Wagibeoni waliamua kujiunga na Waisraeli kwa kuwa walitambua kwamba Mungu alikuwa pamoja nao.

KATIKA SEHEMU HII

Yehova Amchagua Yoshua

Mungu alimpa Yoshua maagizo yanayoweza kutusaidia leo vilevile.

Rahabu Awaficha Wapelelezi

Kuta za Yeriko zilianguka chini. Lakini nyumba ya Rahabu iliendelea kusimama, hata ingawa ilikuwa imejengwa kwenye ukuta.

Yoshua na Wagibeoni

Yoshua alisali kwa Mungu na kusema: “Jua, simama tuli!” Je, Mungu alijibu?

Kiongozi Mpya na Wanawake Wawili Jasiri

Baada ya Yoshua kufa, Waisraeli walianza kuabudu sanamu. Maisha yakawa magumu, lakini Yehova akawasaidia kupitia mwamuzi Baraka, nabii wa kike Debora, na Yaeli!

Ruthu na Naomi

Wanawake wawili ambao walifiwa na waume zao walirudi Israeli. Mmoja kati ya wanawake hao, Ruthu, alienda kufanya kazi mashambani, na huko Boazi akamwona.

Gideoni Aliwashinda Wamidiani

Baada ya Wamidiani kuwakandamiza Waisraeli kwa muda fulani, watu walianza kumwomba Yehova msaada. Jeshi dogo la Gideoni liliwezaje kuwashinda askari 135,000 Wamidiani?

Hana Alisali Apate Mtoto

Elkana, Hana, Penina, na watoto wao walienda kuabudu katika maskani huko Shilo. Wakiwa huko, Hana alisali ili apate mtoto. Mwaka uliofuata, Samweli akazaliwa!

Ahadi ya Yeftha

Yeftha alitoa ahadi gani, na kwa nini? Binti Yeftha alitendaje kuhusu ahadi ya baba yake?

Yehova Azungumza na Samweli

Kuhani Mkuu Eli alikuwa na watoto wawili waliotumikia wakiwa makuhani katika maskani, lakini hawakutii sheria za Yehova. Kijana Samweli alikuwa tofauti kabisa. Usiku mmoja Yehova alizungumza na Samweli.

Yehova Alimfanya Samsoni Awe na Nguvu

Mungu alimfanya Samsoni kuwa Mnadhiri na alimpatia nguvu nyingi sana. Delila alipomnyoa nywele zake, Wafilisti walimkamata.