Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi wa Sehemu ya 6

Utangulizi wa Sehemu ya 6

Wakati Waisraeli walifika mu Inchi ya Ahadi, tabenakulo ikakuwa nafasi kubwa ya ibada ya kweli. Makuhani walifundisha watu Sheria, na waamuzi waliongoza taifa. Hii sehemu inaonyesha namna maamuzi na matendo ya mutu inaweza kuchochea sana wengine wafanye mambo ya muzuri ao ya mubaya. Kila Mwisraeli alipaswa kuwa muaminifu kwa Yehova na kwa watu wengine. Inaonyesha namna Debora, Naomi, Yoshua, Hana, binti ya Yefta, na Samweli walikuwa mifano ya muzuri kwa wengine. Inaonyesha tena kama hata watu fulani wenye hawakukuwa Waisraeli, kama vile Rahabu, Rutu, Yaeli, na Wagibeoni walichagua kuwa upande wa Waisraeli kwa sababu walitambua kama Mungu alikuwa pamoja nao.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 29

Yehova Alichagua Yoshua

Mungu alipatia Yoshua maagizo yenye inaweza kutusaidia leo.

SOMO LA 30

Rahabu Alificha Wapelelezi

Kuta za Yeriko zilianguka. Lakini nyumba ya Rahabu haikuanguka, hata kama ilikuwa imejengwa ku ukuta.

SOMO LA 31

Yoshua na Wagibeoni

Yoshua alisali kwa Mungu na kusema: “Jua, simama bila kutikisika!” Je, Mungu alijibu?

SOMO LA 32

Kiongozi Mupya na Wanamuke Mbili Wenye Uhodari

Kisha Yoshua kufa, Waisraeli walianza kuabudu sanamu. Maisha ilikuwa nguvu, lakini Yehova aliwasaidia kupitia muamuzi Baraka, nabii mwanamuke Debora, na Yaeli!

SOMO LA 33

Rutu na Naomi

Wanamuke wawili wenye bwana zao walikufa walirudia Israeli. Rutu, mumoja kati ya wale wanamuke, alienda kufanya kazi mu shamba, na kule Boazi akamuona.

SOMO LA 34

Gideoni Alishinda Wamidiani

Kisha Wamidiani kutesa Waisraeli, watu walianza kumulilia Yehova awasaidie. Namna gani maaskari kidogo wa Gideoni waliweza kushinda maaskari 135000 Wamidiani?

SOMO LA 35

Hana Anasali Apate Mutoto Mwanaume

Elkana, Hana, Penina, na watoto wao walienda kuabudu ku tabenakulo kule Shilo. Wakati wako kule, Hana anasali apate mutoto. Mwaka wa kufuata, Samweli anazaliwa!

SOMO LA 36

Ahadi ya Yefta

Yefta alitoa ahadi gani, na juu ya nini? Binti ya Yefta alifanya nini kisha kujua ahadi ya baba yake?

SOMO LA 37

Yehova Anazungumuza na Samweli

Kuhani Mukubwa Eli alikuwa na watoto mbili wanaume wenye walikuwa makuhani ku tabenakulo, lakini hawakutii sheria za Yehova. Kijana Samweli hakukuwa vile, na Yehova alizungumuza naye.

SOMO LA 38

Yehova Alipatia Samsoni Nguvu

Mungu alipatia Samsoni nguvu mingi juu apigane na Wafilisti, lakini wakati Samsoni alikamata uamuzi wa mubaya, Wafilisti walimukamata.