Utangulizi wa Sehemu ya 7
Sehemu hii inazungumuzia historia ya maisha ya Mufalme Sauli na Mufalme Daudi. Inazungumuzia mambo yenye ilifanyika mu kipindi cha miaka 80 hivi. Ku mwanzo, Sauli alikuwa munyenyekevu na alimuogopa Mungu. Lakini kisha wakati fulani alibadilika na kukataa kufuata muongozo wa Yehova. Yehova alimukataa, na kisha wakati fulani akaambia Samweli atie Daudi mafuta juu akuwe mufalme wa pili wa Israeli. Juu ya wivu, Sauli alitafuta mara mingi kuua Daudi. Lakini, Daudi hakulipiza kisasi. Yonatani, mutoto ya Sauli, alijua kama Yehova alikuwa amechagua Daudi. Kwa hiyo, alichagua kuwa mushikamanifu kwa Daudi. Hata kama Daudi alifanya zambi fulani nzito, aliitika Yehova
amurekebishe. Kama uko muzazi, usaidie mutoto wako ajue kama ni jambo ya maana sana kuwa muaminifu kwa Yehova na kutii wale wenye amechagua juu watuongoze.KATIKA SEHEMU HII
SOMA LA 39
Mufalme wa Kwanza wa Israeli
Yehova alikuwa amepatia Waisraeli waamuzi wa kuwaongoza, lakini wao waliomba wakuwe na mufalme. Samweli alitia Sauli mafuta juu akuwe mufalme wa kwanza wa Israeli, lakini kisha wakati fulani Yehova alikataa Sauli. Juu ya nini?
SOMO LA 40
Daudi na Goliati
Yehova anachagua Daudi akuwe mufalme wa pili wa Israeli, na Daudi anaonyesha juu ya nini alistahili kuchaguliwa.
SOMO LA 41
Daudi na Sauli
Juu ya nini mwanaume mumoja alichukia mwenzake, na ule mwenye alichukiwa alitenda namna gani?
SOMO LA 42
Yonatani Alikuwa Hodari na Mushikamanifu
Mutoto wa mufalme alikuwa rafiki wa sana wa Daudi.