Utangulizi wa Sehemu ya 8
Yehova alimbariki Sulemani kwa kumpa hekima nyingi na akampa pendeleo la kujenga hekalu. Hata hivyo, hatua kwa hatua Sulemani alimwacha Yehova. Ikiwa wewe ni mzazi, mweleze mtoto wako jinsi waabudu wa sanamu walivyomfanya Sulemani amwasi Mungu. Ufalme uligawanyika na wafalme wabaya wakawafanya watu wawe waasi-imani na kuabudu sanamu. Wakati huo, manabii wengi washikamanifu wa Yehova waliteswa na kuuawa. Malkia Yezebeli aliwafanya watu wa ufalme wa kaskazini watumbukie zaidi katika uasi-imani. Hicho kilikuwa kipindi kibaya sana katika historia ya Israeli. Lakini bado kulikuwa na watumishi wengi waaminifu wa Yehova, kutia ndani Mfalme Yehoshafati na nabii Eliya.
KATIKA SEHEMU HII
Hekalu kwa Ajili ya Yehova
Mungu akubali ombi la Mfalme Sulemani na kumpa mapendeleo mengi.
Ufalme Wagawanyika
Waisraeli wengi waacha kumwabudu Yehova.
Jaribu Kwenye Mlima Karmeli
Mungu wa kweli ni nani? Yehova au Baali?
Yehova Amwimarisha Eliya
Je, unafikiri anaweza kukuimarisha pia?
Mwana wa Mjane Afanywa Kuwa Hai Tena
Miujiza miwili katika nyumba ileile!
Malkia Mwovu Aadhibiwa
Yezebeli anapanga njama ya kumwua Nabothi ili amnyang’anye shamba lake la mizabibu! Yehova Mungu anaona uovu na tendo lake la ukosefu wa haki.
Yehova Amlinda Yehoshafati
Mfalme Yehoshafati asali kwa Mungu Yuda inapotishwa na mataifa adui.