Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi wa Sehemu ya 8

Utangulizi wa Sehemu ya 8

Yehova alibariki Sulemani kwa kumupatia hekima ya mingi na alimupatia pendeleo la kujenga hekalu. Lakini, polepole Sulemani alimuacha Yehova. Kama uko muzazi, ufasirie mutoto wako namna watu wenye walikuwa wanaabudu miungu ya uongo walifanya Sulemani aache kumuabudu Yehova. Ufalme uligawanyika na wafalme wabaya wakafanya watu wakuwe waasi-imani na waabudu-sanamu. Mu ile wakati, manabii wengi washikamanifu wa Yehova waliteswa na kuuawa. Malkia Yezebeli alifanya watu wa ufalme wa kaskazini wakuwe waasi-imani sana. ule ulikuwa wakati wa mubaya sana mu historia ya Israeli. Lakini kulikuwa kungali watumishi wengi waaminifu wa Yehova, sawa vile Mufalme Yehoshafati na nabii Eliya.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 44

Sulemani Anajengea Yehova Hekalu

Mungu alikubali ombi la Mufalme Sulemani na alimupatia mapendeleo makubwa.

SOMO LA 45

Ufalme Unagawanyika

Waisraeli mingi wanaacha kumuabudu Yehova.

SOMO LA 46

Mambo Yenye Ilifanyika Kwenye Mulima Karmeli

Nani njo Mungu wa kweli? Yehova ao Baali?

SOMO LA 47

Yehova Alitia Eliya Moyo

Unawaza kama anaweza kukutia moyo na wewe?

SOMO LA 48

Mutoto wa Mujane Anafufuliwa

Miujiza mbili mu nyumba ileile!

SOMO LA 49

Malkia Muovu Anapata Malipizi

Yezebeli anafanya mipango ya mubaya ya kumuua Naboti juu amunyanganye shamba lake la mizabibu! Yehova Mungu anaona uovu wa Yezebeli na tendo lake la kukosa haki.

SOMO LA 50

Yehova Anasaidia Yehoshafati

Yehoshafati mufalme muzuri anasali kwa Mungu wakati mataifa adui inaogopesha Yuda.