Utangulizi wa Sehemu ya 8
Yehova alibariki Sulemani kwa kumupatia hekima ya mingi na alimupatia pendeleo la kujenga hekalu. Lakini, polepole Sulemani alimuacha Yehova. Kama uko muzazi, ufasirie mutoto wako namna watu wenye walikuwa wanaabudu miungu ya uongo walifanya Sulemani aache kumuabudu Yehova. Ufalme uligawanyika na wafalme wabaya wakafanya watu wakuwe waasi-imani na waabudu-sanamu. Mu ile wakati, manabii wengi washikamanifu wa Yehova waliteswa na kuuawa. Malkia Yezebeli alifanya watu wa ufalme wa kaskazini wakuwe waasi-imani sana. ule ulikuwa wakati wa mubaya sana mu historia ya Israeli. Lakini kulikuwa kungali watumishi wengi waaminifu wa Yehova, sawa vile Mufalme Yehoshafati na nabii Eliya.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 44
Sulemani Anajengea Yehova Hekalu
Mungu alikubali ombi la Mufalme Sulemani na alimupatia mapendeleo makubwa.
SOMO LA 49
Malkia Muovu Anapata Malipizi
Yezebeli anafanya mipango ya mubaya ya kumuua Naboti juu amunyanganye shamba lake la mizabibu! Yehova Mungu anaona uovu wa Yezebeli na tendo lake la kukosa haki.
SOMO LA 50
Yehova Anasaidia Yehoshafati
Yehoshafati mufalme muzuri anasali kwa Mungu wakati mataifa adui inaogopesha Yuda.